
Mwenyekiti
wa Klabu ya Yanga Fc, Yusuph Manji leo amefunguka kuhusu taarifa za
uwepo wa mgogoro wa eneo alilolitoa kwa ajili ya ujenzi wa uwanja wa
mazoezi wa klabu hiyo lililopo Gezaulole na kusema kuwa eneo hilo halina
mgogoro na kwamba wakati wowote wanachama wa klabu hiyo wakimpa ridhaa,
ujenzi wa uwanja huo utaanza baada ya siku tisini.
Manji
ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu
maandilizi ya mkutano mkuu wa klabu hiyo unaotarajiwa kufanyika Oktoba
23, 2016.
Amesema
kuwa, hati ya eneo hilo imeandikwa jina la Kampuni yaani Yanga Yetu,
pia amefafanua kuwa eneo litakalotumika kwa ajili ya ujenzi wa uwanja
huo haliko katika mgogoro wowote.
“Uwanja
wa mazoezi utaanza kujengwa ndani ya siku tisini pindi wanachama
wakituruhusu, na ujenzi wake hautachukua zaidi ya miezi nane,” amesema
Manji.
Amesema
kuwa “Nataka uwanja wa mpira na mazoezi ujengwe tofauti, natumaini
wanachama wa Yanga watanikubalia ombi langu ili nianze ujenzi mapema.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment