Rais wa Afrika Kusini anayekumbwa na
kashfa Jacob Zuma, ameondoka kwenye mkutano wa siku ya kimataifa ya
wafanyazi baada ya kukemewa na wafanyakazi wanaomtaka ajiuzulu.
Fujo zilizuka kati ya wafuasi wa Bwana Zuma na wapinzani na kusabababisha hotuba yake kufutwa.
Chama
kikuu cha wafanya kazi Cosatu, kilimtaka Bwana Zuma ajiuzulu mwezi
uliopita baada ya kumfuta kazi waziri wa fedha alijekuwa akiheshimiwa
sana.Bwana Zuma ameapa kusalia ofisini hadi muhula wake ukamilike mwaka 2019

Maandamano yamekuwa yakifanyika kumtaka Zuma ajiuzulu
Alionyeshwa na runinga akiondoka jukwaani kwa hasira na kuondolewa na magari kutoka kwa mkutano ulioandaliwa mjini Bloemfontein
Maafisa wa vyeo vya juu wa ANC nao walikemewa kwenye mkutano uliofanyika mjini Durban.Shinikizo za kumtaka Zuma ajiuzulu zimekuwa zikoongezeka tangu amfute kazi waziri wa fedha Pravin Gordan mwezi Machi.
Maafisa wa vyeo vya juu wa ANC nao walikemewa kwenye mkutano uliofanyika mjini Durban.Shinikizo za kumtaka Zuma ajiuzulu zimekuwa zikoongezeka tangu amfute kazi waziri wa fedha Pravin Gordan mwezi Machi.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment