June 13, 2017

Morocco yatuma ndege za chakula Qatar 

Wiki moja  baada ya baadhi ya nchi za Gu-huba kutangaza kusitisha ushirikiano na Qatar Morocco yatuma ndege za chakula
Saudi Arabia Falme za kiarabu, Bahrein, Misri  zilitangaza kusitisha ushirikiano wa kidiplomasia na Qatar.
Kufuatia mzozo huo huo Morocco imechukua uomuzi wa kujiunga na Qatar na kutuma ndege za chakula nchini Qatar ili kukidhi mahitaji ya raia.
Qatar imewekewa vikwazo na mataifa jirani iikituhumiwa kuunga mkono ugaidi.
Tangazo lililotolewa na ofisi ya waziri wa mambo ya nje wa Morocco lilisema kuwa hatua ya Morocco ya kutuma ndege hizo za chakula imechukuliwa na mfalme Mohammed VI.
Tangazo hilo lilikumbushia kuwa mshikamano unatolewa wito hasa katika mwezi wa Ramadhan katika umma wa kiislamu.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE