July 20, 2017

Image result for tundu lissu
Mbunge Tundu Lissu.
Rais wa Chama cha wanasheria Tanganyika  na  Mwanasheria wa CHADEMA Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amekamatwa na polisi Uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es Salaam leo wakati akielekea nchini Rwanda kwenye kikao cha halmashauri ya EALS kinachotarajiwa kuanza kesho.
 Kamanda wa Polisi kikosi Uwanja wa Ndege Martin Otieno  amethibitisha kukamatwa kwa kiongozi huyo na kudai kuwa amepelekwa makao Makuu ya Polisi japo hakuweza kuweka wazi sababu zilizopelekea kiongozi huyo kukamatwa. 
Tundu Lissu jana akiwa Dodoma aligoma kutoka katika chumba cha mahakama akidai kuwa alikuwa na taarifa za jeshi la polisi kutaka kumkamata baada ya siku kadhaa zilizopita kutoa maoni yake juu ya serikali ya awamu ya tano na Rais. Hata hivyo kiongozi huyo jana aliweza kuondoka Dodoma baada ya kuthibitishiwa kuwa polisi Dodoma walikuwa hawana mpango wowote wa kutaka kumkamata.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE