Msanii wa muziki Dogo Janja (kushoto) na Irene Uwoya (kulia)
Msanii wa muziki wa bongo fleva, Dogo Janja kwa mara ya kwanza
amefunguka kuhusu mahusiano yake, na kutoa sintofahamu kuhusu kutoka
kimapenzi na muigizaji wa filamu za kibongo Irene Uwoya.
Akizungumza
na mtandao wa East Africa Television, Dogo Janja ambaye mara nyingi
hapendi kuzungumzia maisha yake binafsi, ameamua kusema kuwa msanii huyo
anafaa.
"Irene ni mwanamke mzuri, anavutia, kila mwanaume anayejua mwanamke
mzuri anafaa kuwa naye, ila kwa upande wangu mimi namkubali sana Irene
Uwoya, kwani anaigiza vizuri, hivyo namkubali kwa kazi zake pia",
alisema Dogo Janja.
Hivi karibuni kumekuwa na tuhuma za Irene Uwoya kuwa na mahusiano ya
kimapenzi na msanii Dogo Janja, ambapo watu wengi wamekuwa na mtazamo
tofauti wakisema si sahihi kwani Irene Uwoya kwa kuwa ni ni mkubwa sana
kwa Dogo Janja. Jambo ambalo Dogo Janja anaonekana kutoliafiki.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment