September 28, 2017

  

Wasanii wakongwe kwenye game ya muziki ambao ni ndugu wa familia moja Unique Sisters, wamesema wamerudi rasmi kwenye game, kutokana na maombi ya mashabiki na kuachia kazi yao mpya kwa ajili yao inayoitwa 'Kwako wewe'.
Wakizungumza na mwandishi wa East Africa Television, mmoja wa wasanii wanaounda kundi hilo Rahima ambaye ndiye mkubwa wao, amesema walikuwa kimya kutokana na majukumu ya kifamilia, ambapo wawili miongoni mwao wameshaolewa, lakini wameona kiu ya mashabiki imekuwa kubwa.
“Tulikuwa tunapata maoni kutoka kwa mashabiki tuko kimya sana tukasema tunataka kurudi, tulikuwepo na tumerudi, tumerudi kuonyesha kipaji chetu ili kuwafurahisha mashabiki wetu, sio kushindana na mtu yeyote”, amesema Rahima.
Akiendelea kuelezea hayo Radhina ambaye ndiye mdogo kwenye kundi hilo amesema pia wamekuja kuleta ladha tofauti ya muziki, ili kuleta changamoto zaidi kwenye game upande wa wanawake.
“Na pia ni vizuri kuwa na vitu tofauti, vionjo tofauti na watu tofauti ambao wanafanya muziki, ndio maana tumerudi ili kutoa 'option' hiyo, kuna mwengine ataimba kwa vingine, kwa hiyo tutoe 'option' kwa mashabiki waweze kupata vitu vingi na vionjo vingi vya kusikiliza kutoka kwa wanawake”, amesema Radhina.
Pia wasanii hao wameendelea kwa kusema kwamba wamefurahi kuona jinsi game ilivyobadilika siku hizi na kuwa na wasanii wengi wa kike, tofauti na kipindi cha nyuma ambapo wasanii wa kike walikuwa wachache.
“Tunafurahi kwamba wanawake tumejitokeza sasa hivi kwa sababu nakumbuka miaka ya zamani tulikua tyunajaribu sana kuwaita wanawake, sasa hivi watu wamesikia wamejitokeza”, amesema Rahima.
Kundi hilo mla Unique Sisters linaundwa na ndugu wa familia moja, Rahima Kipozi, Radhia Kipozi na Radhina Kipozi.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE