September 28, 2017

 

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amefunguka na kusema kuwa endapo watashindwa kufanya maandalizi mazuri ya michuano ya mataifa ya Africa (AFCON) kwa vijana 2019 basi Watanzania hawawezi kumuelewa.  

Mwakyembe amesema kuwa Tanzania ndiyo iliomba kuwa mgeni wa michuano hiyo mwakani hivyo wanapaswa kufanya maandalizi ya kutosha ili waweze kufanya vizuri katika michuano hiyo na kusema kama hawatafanya maandalizi mazuri basi watachekesha. 
"Ndugu zangu hatuna sababu kabisaa za kutojiandaa vizuri tutachekesha na hamtatusamehe Watanzania tukishindwa kujiandaa vizuri, nashukuru sana kwamba na timu nzuri sana na tulianza muda mara tu baada ya uchaguzi yapo mambo mengi sana kuhusu suala hili lakini uzuri ni kwamba tumeanza kuyangalia kuhusu viwanja vya mazoezi, masuala ya usafiri, usalama hata maandalizi ya timu yetu yenyewe nayo ni mchakato mkubwa" alisema Mwakyembe 
Aidha Mwakyembe amesema kuwa katika kipindi kilichobaki anaamini kuwa watafanya maandalizi makubwa sana 
 

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE