Mtoto wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania marehemu, Edward
Moringe Sokoine, Kereto Sokoine ameauwa kwa kuchomwa kisu katika ugomvi
ulitokea na mkewe hii leo mkoani Arusha.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, amethibitisha
kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa limetokea mchana wa leo
Jumatano,na jeshi la polisi tayari lipo katika eneo la tukio kufuatilia
kwa undani kilichojiri mpaka kutokea kwa tukio hilo.
Chanzo: Mtanzania
0 MAONI YAKO:
Post a Comment