Muigizaji Elizabeth Michael (Lulu), amesema kesi inayomkabili ya kuua
bila ambayo inamkabili haikuwahi kuisha kama baadhi ya watu
wanavyodhani.
Muigizaji huyo huyo anakabiliwa na kesi ya kusababisha kifo bila
kukusudia cha aliyewahi kuwa muigizaji mwenzie, Steven Kanumba
kilichotokea April 7, 2012 . Akizungumza na Planet Bongo ya EA Radio
ameeleza kuwa watu wanadhani kesi hiyo ilimalizika kutokana na kutojua
sheria.
“Unajua watu hawajui sheria, kesi haikuwahi kuisha ni procedure ya
kawaida ya mahakama imefuatwa na ni muda wake umefika sasa, siyo kama
imeibuka tu” amesema Lulu.
“Kwa sababu mimi ndiye muhusika nimepata taarifa kwa njia ya kisheria
siyo kama nyie kwenye mitandao, pengine niliipata kabla yenu”
ameongeza.
Hata hivyo amesema kuwa asingependa kulizungumzia sana suala hilo
kutokana tayari lipo mahakamani ila amelazimika kufanya hivyo kutokana
yeye ndiye muhusika. Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa tena hapo kesho
October 19, 2017.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment