October 10, 2017


 

Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga ametangaza kujiengua kwenye kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu ambao umepangwa kufanyika tarehe 26 Oktoba mwaka huu.
Bwana Odinga amesema anataka kufanyike uchaguzi mpya wa haki na halali kama ilivyoamuliwa na mahakama ya juu mapema mwezi septemba.
Akitaja sababu za kujiondoa, Odinga amesema amejiondoa ili kuipa tume ya uchaguzi nchini humo (IEBC) muda wa kutosha kufanya mabadiliko ambayo yatawezesha kufanyika uchaguzi kwa njia iliyo huru.
Uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika tarehe 26 Oktoba mwaka huu, utakuwa ni marudio ya uchaguzi mkuu, baada ya mahakama ya juu nchini Kenya kufuta matokeo ya uchaguzi wa tarehe 8 mwezi Agosti mwaka huu.
Matokeo ya awali ya tume ya uchaguzi yalimtangaza Rais Uhuru Kenyatta kuwa mshindi.

Related Posts:

  • Sepp Blatter akwezwa    Rais wa shirikisho la soka duniani Sepp Blatter amefananishwa na manabii waliopita, kama vile rais wa zamani wa Afrika kusini hayati Nelson Mandela pamoja na Winston Churchill wakati wanachama kumi wa shiri… Read More
  • Wale mashabiki wa Msaga Sumu, hii inawahusu sana watu wangu   Kwa style yake ya kuimba imemfanya awe Mfalme wa Uswahilini, Wanamuita Msaga Sumu huku kwetu uswahili tunamjua sana si jambo la kushangaa maeneo ya Chamwino,Mafisa, Msamvu, Kichangani, Mwembesongo na mpaka sasa a… Read More
  • Waislamu watakiwa kujiepusha na uvunjaji amani Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini, Ernest Mangu na viongozi wa dini ya Kiislamu nchini, wameungana kwa pamoja na kukemea vitendo vya uhalifu. Viongozi hao wamezitaka familia kutoa malezi bora kwa watoto wao ili … Read More
  • Wageni waendelea kushambuliwa A Kusini   Kumekuwa na mashambulizi zaidi usiku dhidi ya biashara zinazomilikiwa na raia wa kigeni nchini Afrika Kusini. Polisi walitumia gesi ya kutoa machozi na risasi za mipira kutawanya umati kusini mwa mji wa Johannesbu… Read More
  • Mwanzilishi wa IS auawa nchini Iraq    Al-Douri  Runinga nchini Iraq imeripoti kuwa Izzat Ibrahim al-Douri, ambaye wakati mmoja alikuwa makamu wa Rais Saddam Hussein na ambaye alitajwa kama nguzo kuu katika mchipuko wa kundi la Islamic Sta… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE