Muongozaji wa video nchini Tanzania, Msafiri Shabani maarufu Travela wa kampuni ya Kwetu Studios, ameeleza mipango yake katika mwaka 2018.
Akiongea na TVE katika kipindi cha Eight, Travela amesema alikuwa na
ndoto za kufanya kazi na wasanii wa nje katika mwaka huu ambapo tayari
ameshapata dili kutoka kwa wasanii kumi mpaka sasa.
“Mwaka jana nilikuwa na dream kuwa mwaka huu lazima nifanye video na
wasanii wa nje. Mpaka sasa kuna wasanii kama kumi wa nje ambao nataka
nifanye nao,” amesema muongozaji huyo wa video.
Akiongea kuhusu watu wanavyozungumza video zake kukosa stori, Msafiri
amesema hilo linatokana na tatizo kubwa la mashabiki wengi wamekuwa
wakitengeneza script zao vichwani kabla ya video ya wimbo haijatoka.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment