June 02, 2018

Image result for mapacha walioungana wafariki
Mabinti mapacha walioungana, Maria na Consolata Mwakikuti, wamefariki dunia katika hospitali ya mkoa wa Iringa walikokuwa wakitibiwa. Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela ameandika kupitia mtandao wake wa Twitter. Kwa wakati fulani mapacha hao walitibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kabla ya kurejeshwa Iringa ambako hali yao haikuimarika na mauti kuwakuta. Mabinti hao waliokuwa wakisoma chuo cha Ruaha Catholic University mjini Iringa wamefariki majira ya saa moja usiku wa Jumamosi.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE