Watoa huduma
wa afya wametakiwa kufanya kazi kwa ufanisi ili kuepukan na vifo vya akina mama
wajawazito na watoto wachanga ili kuhakikisha takwimu za vifo vya akina mama
wajawazito haziongezeki kama ilivyo sasa
kwani takwimu zinaonyesha vifo vya akina mama vimeongezaka kutoka 454
katika vizazi hai laki moja kwa mwaka
jana hadi kufikia vifo 556 kwenye vizazi
hai laki moja.
Rai hiyo
imetolewa na mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk, Frank Jacob katika mkutano wa
kuwajengea uwezo watoa huduma za Afya kutoka
Zahanati na Vituo vya Afya 20 Mkoani Morogoro
ambapo amesema ili kupunguza vifo vya akina mama wajawazito nilazima wataalamu wa Afya wafate vigezo vya
utoaji wa huduma bora kama kuangalia madhurio ya akima mama Clinic, kutoa dozi
ya pili (ASP) ya kukinga Maralia , Madini ya chuma na Folic Acid kwa mjamzito pamoja na kutoa elimu kuhusu uzazi wa mpango
ambao pia hupunguza vifo vya akina mama kwa asilimia 44.
Mafunzo hayo
ambayo yanatoa nafasi kwa watoa huduma kutoka katika Zahanati na Vituo vya Afya
kuweza kutoa huduma za dharula kwa mama mjamzito na mtoto wamebaisha changamoto
mbalimbali ikiwemo ya jinsi ya kutoa huduma kwa mama wenye vifafa vya mimba na
wale ambao wanatokwa damu nyingi baada ya kujifungua huku tatizo la usafiri
vijiji nalo limeonekana kuwa sehemu ya changamoto.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment