July 29, 2018

Image result for Happyness Seneda 
Aliyekuwa mkuu wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani bi. Happyness Seneda, amewaaga wananchi wa Kisarawe huku akiwataka waoneshe ushirikiano kwa mkuu mpya wa Wilaya hiyo bi. Jokate Mwegelo. katika ukurasa wake wa Facebook. Happyness Seneda ameandika

 
Kwa heshima kubwa ninamshukuru Mungu kwa yote anayoendelea kufanya katika maisha yangu,, najua ni kwa neema yake tu si kwa ujanja wala ubora!! Pia ninamshukuru mhe Rais kwa kuendelea kuniamini.
Ndugu zangu wana Kisarawe, wa ukae ninawashukuru sana kwa ushirikiano mlionipa tokea siku ya kwanza nakanyaga ardhi ya Kisarawe mpaka muda huu ambao Mhe. Rais imempendeza mimi kuhamia kituo kingine cha kazi na kwa nafasi nyingine!! Kwa umoja wetu tulifanya mengi na tulipanga kufanya mengi!!
Kwa kweli nitawamiss sana sana, Mungu awabariki sana endeleeni kudumisha umoja, mshikamano na ushirikiano bila kujali dini, itikadi wala kabila na hakika Mungu atafanya makubwa katika wilaya ya Kisarawe.
Ninaomba mumpatie ushirikiano zaidi ya huu ndugu yangu Jokate Mwengelo, kwa kufanya hivyo Kisarawe itaendelea kwa kasi kubwa.
Mungu ibariki Kisarawe🙏🙏
HODI IRINGA

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE