Gari la Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Manyara, Mhe. Anna Gidarya
limeshambuliwa kwa kupigwa risasi kwenye matairi ya mbele na nyuma ya
ubavu mmoja muda mfupi uliopita akiwa katika kata ya Majengo, Monduli
mkoani Arusha.Taarifa zilizotolewa na chama hicho, zimeeleza kuwa gari hiyo
imeshambuliwa leo asubuhi, hata hivyo haijulikani ni watu gani
walioshambulia gari hilo.
Hata hivyo, Kamanda wa polisi mkoa wa
Arusha, Ramadhani Ng’anzi, amesema hana taarifa juu ya tukio hilo,
anachojua ni kuwa kwa sasa hali ya uchaguzi wilayani Monduli ipo safi.
Wakati hilo likitokea, Mawakala wa CHADEMA kata ya Esilalei wote wametolewa nje kwa kukosa fomu za kiapo.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment