August 27, 2012


Msanii Peter Mponeja a.k.a C-SIR MADINI (SISA), jana (26th Aug 2012) ameshot video ya wimbo wake mpya kabisa ambao bado haujawa released alioamua kuupa jina la PAIN KILLER. Video imefanywa jijini Dar es Salaam na kampuni ya Next Level chini ya director Adam Juma. 

Hii itakua ni video ya tatu kwa msanii huyu mwenyeji wa jiji la Mwanza baada ya mbili zilizoishatangulia kutoka ambazo ni KIFUNGO HURU aliyoitoa mwezi may 2011, pamoja na NISHIKE MKONO aliyoitoa April mwaka huu. 

Katika video hii ya Pain Killer, C-sir Madini amevalishwa na KIDOTI FASHION ya mrembo JOKATE ambayo imeshavalisha wasanii wengi wa bongo kama Diamond na Ommy Dimpoz kwenye video yake mpya ya Baadae.

Video ya C-sir inategemewa kuwa hewani muda wowote mwezi September 2012, na wiki moja baadea  itafuatiwa na audio katika radio stations zote. 

Fuatilia picha za maandalizi na wakati wa kushot video ya Pain Killer.

C-sir akiwa salon
Jokate na C-sir Madini

Location,wakati wa makeup

Video Model
Dancers wakipewa maelekezo na director

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE