October 07, 2012



STAMINA  inasemekana  ndiye  msanii  wa  kibongo  aliyefunika.

 
Rick Ross hapa akiwaelekeza jambo mashabiki hawapo pichani wakati alipokuwa akiimba jukwaani usiku huu.

Msanii wa miondoko ya rusha rohoo a.k.a Miduara,Shilole akijiachia jukwaani
 
Rick Ross akiendelea kupagawisha mashabiki wake usiku huu kwenye viwanja vya Leaders
 
Watu wa usalama wakijaribu kudhibiti rapsha zilizokuwa zikijitokeza  kutokana na mashabiki wengi kuwa na hamu ya kumuona mwanamuziki Rick Ross
 
Bibi Cheka na Stiko kutoka pande za TMK nao wakafanya mambo makubwa,
 
Wadau kutoka Serengeti wakifyurahia jambo katika burudani ya muziki.
 
Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko SBL Ephraim Mafuru na kutoka kushoto Meneja wa Masoko SBL Emmilian Rwejuna na Mdau Rawlence Mafuru pamoja na wadau wengine wakipozi kwa picha.
Wadau mbalimbali wakifuatilia burudani ya mwanamuziki Rick Ross wakati alipokuwa akitumbuiza,
Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti SBL Bw Ephraim Mafuru akitangaza mshindi wa bahati nasibu ya magari mawili kwa mkoa wa Dar es salaam iliyoendeshwa katika matamasha yote ya Serengeti Fiesta mwaka huu kutoka kulia ni Bw. Mrisho kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha , Rugambo Rodney Meneja masoko wa Push Mobile na kushoto ni Mkurugenzi wa Clouds Entarteinment Bw Joseph Kusaga wakishuhudia tukio hilo
 
Pichani chini na juu mashabiki wakishangilia kwa nguvu wakati wanamuziki huyo akiimba jukwaani
Rachel Mwanamuziki wa Bongofleva kutoka kundi la THT akicheza na mmoja wa wacheza shoo wake  katika Tamasha la Serengeti Fiesta linalofanyika usiku kuu kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam ambapo pamoja na wasanii mbalimbali wakali wa nyumbani, mwanamuziki maarufu wa Hiphop kutoka nchini Marekani Rick Ross “The Boss” atahitimisha tamasha hilo kwa shoo kali usiku huu.
 
Rachel na wacheza shoo wake wakiburudisha mashabiki viwanja vya Leaders jijini Dar es salaal katika tamasha la Serengeti,
 
RaSasa ni zamu ya Lina wa THT akiwa jukwaani akiimba wimbo wake wa nampenda ambao umewafanya mashabiki wa muziki kuitikia kwa nguvu wakati akiwaimbisha hapa akipozi kwa staili ya aina yake huku akiwaimbisha mashabiki wake
Mwanamuziki DYNA  akiimba katika Tamasha la Serengeti Fiesta linalofanyika usiku kuu kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam
 
DAYNA akibenwa juujuu na wacheza shoo wake wakati akifanya vitu vyake jukwaani katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012
 
Wadau kutoka kampuni ya bia ya Serengeti wakishoo love katika tamadsha hilo.
 
Mdau Edward na maiwaifu waki wakipozi kwa picha
 
Barnaba akikamua jukwaani katika tamasha la Serengeti Fiesta usiku huu.
 
DAYNA  akimwaga mauno jukwaani wakati akiimba jukwaani usiku huu katika tamasha la Serengeti Fiesta.



Dayna  Mkali wao na wakali wao classic on stage fiesta dar 2012. thnx kwa ushilikiano wapendwa.

 
Michael Jackson wa Bongo akifanya vitu vyake mbele ya mashabiki wake alivuta hisia za wengi kutokana na kuigiza uchezaji wa marehemu Michael Jackson wa Marekani, pichani ni nyomi ya mashabiki waliojitokeza katika tamasha hilo kwenye viwanja vya Leaders
 
Msanii Aika kutoka kundi la muziki wa Bongofleva la Per One akifanya vitu vyake jukwaani katika shoo za utangulizi
 
Wasanii ha wa nao wamefanya mambo makubwa katika tamasha la Serengeti Fiesta 2012 usiku huu kwenye viwanja vya Leaders.
 
Kutoka kushoto ni Rachel, Lina na Daina wote kutoka THT wakiwa tayari kwa kazi ya kuburudisha mashabiki wa Tamasha la Serengeti Fiesa 2012.
 
Umakini kubwa kutoka kwa mashabiki kama wanavyoonekana katika picha
 
Mashabiki wakidatishwa na burudani za mwanzo za tamasha la Serengeti Fiesta usiku huu kwenye viwanja vya Leaders.
Mtangazaji wa Clouds kipindi cha Amplifire Milad Ayo kulia akipozi kwa picha na mdau kutoka Gazeti la Babkubwa .
 
Msanii Aika kutoka kundi la Per One akifanya vitu vyake jukwaani na wasanii wenzake.
Jeshi  la polisi  nalo  lilikuw amakini  sana  katika  shoo  hiyo. 

 Mkali mwingine wa miduara AT na madansa wake wakilishambulia jukwaa.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE