October 27, 2012


Lord Eyes

 Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi wa Kinondoni Charles Kenyela amethibitisha jeshi lake kumshikilia msanii Lord Eyes ambae toka weekend iliyopita taarifa zake zimesambaa baada ya kushutumiwa kuhusika na wizi wa vifaa mbalimbali kwenye gari la mwimbaji Ommy Dimpoz.

Namkariri Charles Kenyela akisema “ni kweli Isaac Waziri Maputo mwenye umri wa miaka 28 alikamatwa tarehe 20 mwezi wa kumi usiku maeneo ya Kinondoni, kukamatwa kwa mtuhumiwa huyu ni kutokana na taarifa tulizozipata kupitia kwa binti mmoja aitwae Kurushinde Hillary (22) mwenye asili ya kiburushi lakini mkazi wa Mwananyamala kwa Makoma Dar es salaam, alikamatwa siku hiyo hiyo kabla ya Lord Eyes”

“Alikamatwa kuhusiana na matukio ya wizi kwenye magari yani kuna mtindo ambao umeibuka ambapo ukipaki gari yako gari nyingine ya wezi inakuja inapaki jirani na gari yako ambapo kwa muda mfupi wanafanya utundu wao wanaoujua, wanafungua gari na kuiba mali iliyoko ndani, mara baada ya huyu binti kukamatwa katika kuhojiwa mtandao wake anaoshirikiana nao alimtaja mtuhumiwa Isaac Waziri Maputo (Lord Eyes)” – Kamanda Kenyela

Kwenye sentensi nyingine Kamanda Kenyela amesema “watu wengi wamelalamika kuibiwa laptop zao, mabegi, mifuko na hata silaha kwa maana mtu anakua anajiamini anaacha kwenye gari akiamini kwamba ameshalock lakini watu hawa na mtandao wao wamekua ni hatari kiasi kwamba wameliza watu wengi”

“Watuhumiwa hawa wawili Kurushinde na Lord Eyes tunawashikilia kwa tuhuma zipatazo 30, yani matukio mbalimbali 30 pengine yanaweza yakaongezeka ambayo yameripotiwa kutokea katika maeneo mbalimbali kama vile Mlimani City, Kijitonyama, ufukwe wa bahari kama Coco beach, kwenye kumbi mbalimbali za starehe na pia  kwenye maeneo ambayo kunakua na harusi, sehemu ambazo kunakua na magari mengi watu hawa ndio huwa wanaitumia hiyo nafasi kufanya uhalifu, tunawashikilia kwa makosa ya wizi”



Hii  ni  kwa  hissani  ya:www.bongoflavortz.com

Related Posts:

  • Hii ndiyo Albam inayoongoza kwa mauzoKumbukumbu za kumuezi david Bowie Albamu ya Black starya gwiji wa muziki Marehemu David Bowie inaongoza kwa mauzo nchini marekani baada ya kutolewa siku mbili kabla ya kifo chake. Albamu hiyo imeuza kopi 181,000 na hivyobasi … Read More
  • Venus Williams apigwa chini katika tenisiKonta ameorodheshwa nambari 47 duniani Mchezaji nyota wa tenisi kutoka Uingereza Johanna Konta amemshinda Venus Williams 6-4 6-2 na kufika raundi ya pili ya shindano la tenisi la Australian Open mjini Melbourne. Konta, 24, al… Read More
  • Ashtakiwa kwa kusambaza picha whatsapp         Miili ya kwanza ya wanajeshi waliouawa Somalia iliwasili Nairobi Jumatatu Mwanamume mmoja nchini Kenya ameshtakiwa kusambaza picha alizodai ni za wanajeshi wa Kenya waliouawa … Read More
  • Nahreel kamkatalia Mkenya Producer maarufu wa Tanzania kwenye muziki wa bongoflevaNahreel ameingia kwenye top stories za leo kwenye Dstv.com baada ya kukataa kumpa beat yake staa mmoja wa hip hop nchini Kenya. Nahreel ambaye mikono yak… Read More
  • Pitio la Magazeti ya leo jumanne january 19, 2016 Karibu mwana familia wa ubalozini.blogspot.com, Leo hii January 19,2016 siku ya jumanne tunakupa tena fursa ya kupitia magazeti yetu ya leo kama yalivyotufikia na kubeba habari zenye uzito wa juu. … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE