December 04, 2012

                APOTEZA  FAHAMU  UKUMBINI

                                                       BERENIKI KIMILO AKIFURAHI JAMBO
 
 
Shindano la Maisha Plus limefikia tamati huku mwana dada Bereniki Kimiro akiibuka mshindi na kujinyakulia Shilingi Milioni 20 za Kitanzania kibindoni.

                                                    Hii ni  5 bora

Nafasi ya pili katika shindano hilo lililo waweka vijana katika kambini ni Venance Mushi amejishindia Tshs. Million 6 huku nafasi mshindi wa Tatu ni Justine Bayo, amejishindia Tshs. Million 4.

Mara baada ya kutangazwa mshindi,  Mshindi wa Maisha Plus 2012, Beneriki alimshuukuru Mungu kwa ushindi, na kusema kuwa ‘yeye si kitu kwa wenzake, hilo ni zali tu’..

Aidha amemshukuru baba yake mzazi kwa kumshauri kusali,a mewashukuru pia wapenzi watazamaji kwa kumpiga kura, ameahidi kuendeleza kile alichokianza kijijini na kuitendea haki nchi yake.. 

Bereniki amemshukuru babu wa Kijijini, Brother Masoud na Crew nzima ya Maisha Plus.. Amemshukuru pia mwanae Kelvin (6yrs) kwa kuvumilia kipindi chote bila kuongea na mama.

Amesema Mungu amejibu maombi yake kwani ukipiga goti, maombi yako yatajibiwa.
 
                                                        Alipata  nafasi  ya  kuzungumza

 
                                           Akisaidiwa  baada  ya  kupoteza  fahamu

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE