December 09, 2013

    Mwanamuziki wa Bongo Freva toka mkoani Morogoro Dayna Nyange ameandika ujumbe wake juu ya kifo cha mzee Nelson Mandela.
    Katika AC yake ya Facebook Dayna ameandika

Tusiishie kumlilia Mzee wetu Nelson Mandela bali tukae tukimuombea apumzike kwa amaini, Tusimkumbuke kwa maneno bali tumkumbuke na kumuenzi kwa vitendo vyake.Alihitaji wa Afrika kuwa hutru lakini hakung'ang'ania madaraka. Alihitaji usawa kwa watu wote, hakuwa mbaguzi kwa kipindi chake chote. Hakuwahi kujitenga na wengine. Alikuwa radhi kumwaga damu yake kwa ajili ya wengine mfano pale alipotumikia kifungo cha miaka 27 jela kwa ajili ya uhuru wa Afrika kisini. Ana mengi sana ambayo hatuwezi kuyataja yote lakini Mandela ni mfano wa kuigwa. Mungu ailaze roho yake mahali pema Peponi.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE