December 09, 2013


 
Madole ambaye kwa sasa ni Meneja NMB Mt. Uluguru Br.
  WACHEZAJI wa klabu ya Morogoro Veteran wamempongeza Mwenyekiti wao, Hamis Madole (Mboma) kwa kuhitimu shahada ya pili ya corporate managenment (MBA) katikachuo kikuu cha Mzumbe huku wakimtaka kuongeza juhudi katika utendaji kazi mkoani hapa.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi katika mjini hapa kwa niaba ya wachezaji wenzake aisema kuwa shahada ya pili aliyotunukiwa katika chuo kikuu cha Mzumbe anapaswa kuongeza juhudi hasa katika utendaji kazi na kuleta ubunifu kutokana na elimu hiyo.
 
Hamis Madole akifurahia jambo na washambuliaji zamani wa klabu ya Pamba ya Mwanza, Mtibwa Sugar na Moro United, Ally Bushiri kushoto na Boniface Mapunda aliyewahi kuichezea klabu ya daraja la pili ya SUA kulia wakati wa hafla ya kumpongeza baada ya kuhitimu shahada ya pili ya corporate managenment (MBA) katika chuo kikuu cha Mzumbe kilichopo wilaya ya Mvomero mkoani hapa
 
Ally Bushiri alisema kuwa (Hamis Madole) ameongeza shahada ya pili na taasisi ambayo anafanyia kazi benki ya NMB ina changamoto kubwa hasa kwa kusaka mbinu mpya za kuwashawishi wateja ili kuweka fedha zao katika benki hiyo ambayo inahitaji mbinu mbadala ya kubuni wazo la ushawishi na kuwa kutokana na ushindani mkubwa uliopo ndani ya taasisi hizo za fedha hapa nchini 

 Naye Mwenyekiti huyo, Hamis Madole (Mboma) alisema ushauri huyo ataufanyia kazi na kujitahidi kubuni mbinu mbadala zitakazo wezesha kukabiliana na changamoto mbalimbali zikiwemo zile zinazoimbuka taasisi hiyo hiyo ya fedha kwa kusaka wateja kuweka fedha katika benki hiyo.Wengine ni Mwenyekiti wa chama cha soka la wanawake mkoa wa Morogoro, Edna Lema, Detha Thomas aliyekipiga klabu ya Polisi Moro SC, Ally Shomari Reli Morogoro na Polisi Moro SC, Omari Mkesi Reli Morogoro na Victa Bundara, Yanga Sport Club, Mtibwa Sugar na Polisi Moro

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE