February 15, 2014

 
 Mchezo uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu baina ya vilabu vya Simba na Mbeya City uliokuwa unachezwa hivi punde huko jijini Mbeya katika dimba la Sokoine umemalizika.
Matokeo ya mchezo huo ni sare ya bao moja kwa moja,Mbeya City ndio walioanza kuliona lango la Simba katika dakika ya 17 kwa mkwaju wa penati, bao hilo lilidumu mpaka mapumziko wenyeji wakitoka kifua mbele.
simba-mpya-2
Kipindi cha pili Simba walianza kwa kasi na hatimaye katika dakika ya 50, mshambuliaji hatari wa Simba Mrundi Amiss Tambwe akaifungia timu yake bao la kusawazisha.
Timu hizo ziliendelea kushambuliana lakini mpaka refa anapuliza kipenga cha mwisho matokeo yalibaki moja kwa Mbeya City na moja kwa Simba.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE