March 03, 2014

Dar es Salaam. Wakati Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) likipandisha bei ya umeme kwa zaidi ya asilimia 40, limetakiwa kulipa zaidi ya Sh844.8 bilioni, kwa kampuni zilizoifungulia kesi mbili tofauti kwa kukiuka mkataba wa kukodisha mitambo ya kuzalisha umeme ya Kampuni ya IPTL.

Baada ya shirika hilo kushindwa kesi hiyo, sasa limepoteza pia haki ya kumiliki mitambo ya IPTL ikiwa ni mwaka mmoja tu kabla ya muda wa kuikodisha ufikie kikomo na mitambo hiyo iwe mali ya Tanesco kwa asilimia 100.

Mkataba huo wa kukodisha mitambo hiyo wa miaka 20 ulioingiwa mwaka 1995, ulikuwa ufikie kikomo mwaka 2015.

Kiasi hicho cha fedha ni sawa na kiasi cha fedha ambazo kinapangwa kwa ajili ya bajeti za wizara nyeti nchini.


ZAIDI: .udakuspecially.com

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE