July 04, 2014

chuji

AZAM FC: HATUJAINGIA MKATABA NA CHUJI, AMEOMBA KUFANYA MAZOEZI Kitaifa

chuji
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
BAADA ya taarifa kuenea mchana wa leo kuwa aliyekuwa kiungo mzoefu wa Yanga, Athumani `Idd Chuji` amesajiliwa na Azam kutokana na kuonekana katika mazoezi ya klabu hiyo kwenye uwanja wa Azam Complex, uongozi wa mabingwa hao umekanusha taarifa hizo.
Chuji aliyetemwa na Yanga alionekana katika jezi ya Azam fc, lakini  msemaji wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga  amesema klabu hiyo haijaingia mkataba wowote na kiungo huyo.
Jafar aliongeza kuwa Chuji aliomba kufanya mazoezi na Azam na kwasababu klabu hiyo inapenda michezo haikuona sababu ya kumnyima nafasi hiyo.
“Chuji aliomba kufanya mazoezi, uongozi ukaona si jambo la busara kumkatalia”. Alisema Jafar.
“Hata katika mazoezi ya leo jezi aliyovaa haikuwa na namba yoyote, kwahiyo hatuna mkataba wowote”.
Jafar alisisitiza kuwa jioni ya leo ameongea na katibu mkuu wa klabu hiyo, Nassor  Idrissa `Father` na alielezwa kuwa hakuna mkataba wowote ambao Azam fc imeingia na Chuji zaidi ya kuomba kufanya mazoezi.
‘Kuvaa jezi ya Azam sio kwamba ndio tumemsajili, sisi tunaenda kisasa. Tunapofanya mazoezi, timu moja inavaa jezi na timu nyingine inavaa jezi. Kama mchezaji yupo mazoezini lazima avae jezi, lakini hatuna mkataba na mchezaji huyo”.
Hata hivyo, Jafar alisema suala la Chuji kusajiliwa itategemeana na mwalimu atamuonaje katika mazoezi na kama ataonekana ana kiwango kizuri, kazi ya uongozi ni kutekeleza mahitaji ya mwalimu.
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=3036#sthash.uxAcf8RE.dpuf

  Na Baraka Mpenja, Dar es salaam 
BAADA ya taarifa kuenea kuwa aliyekuwa kiungo mzoefu wa Yanga, Athumani `Idd Chuji` amesajiliwa na Azam kutokana na kuonekana katika mazoezi ya klabu hiyo kwenye uwanja wa Azam Complex, uongozi wa mabingwa hao umekanusha taarifa hizo.  Chuji aliyetemwa na Yanga alionekana katika jezi ya Azam fc, lakini  msemaji wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga  amesema klabu hiyo haijaingia mkataba wowote na kiungo huyo.  Jafar aliongeza kuwa Chuji aliomba kufanya mazoezi na Azam na kwasababu klabu hiyo inapenda michezo haikuona sababu ya kumnyima nafasi hiyo.  “Chuji aliomba kufanya mazoezi, uongozi ukaona si jambo la busara kumkatalia”. Alisema Jafar.  “Hata katika mazoezi ya leo jezi aliyovaa haikuwa na namba yoyote, kwahiyo hatuna mkataba wowote”.  Jafar alisisitiza kuwa jioni ya leo ameongea na katibu mkuu wa klabu hiyo, Nassor  Idrissa `Father` na alielezwa kuwa hakuna mkataba wowote ambao Azam fc imeingia na Chuji zaidi ya kuomba kufanya mazoezi.  ‘Kuvaa jezi ya Azam sio kwamba ndio tumemsajili, sisi tunaenda kisasa. Tunapofanya mazoezi, timu moja inavaa jezi na timu nyingine inavaa jezi. Kama mchezaji yupo mazoezini lazima avae jezi, lakini hatuna mkataba na mchezaji huyo”.  Hata hivyo, Jafar alisema suala la Chuji kusajiliwa itategemeana na mwalimu atamuonaje katika mazoezi na kama ataonekana ana kiwango kizuri, kazi ya uongozi ni kutekeleza mahitaji ya mwalimu.

Related Posts:

  • Paul Makonda aombewa tena MUFTI wa Tanzania Sheikh Abubakary Zubery amemuombea dua, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na Rais Dk. John Magufuli ili waweze kulitumikia vema taifa na kuliletea maendeleo. Zubery alimfanyia dua hiyo Makon… Read More
  • Fatma Karume: Dk. Shein siyo rais Zanzibar Wakili Fatma Amani Abeid Karume MJUKUU wa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, Abeid Amani Karume, amepinga hatua ya kumtangaza Dk. Alli Mohammed Shein, kuwa rais Visiwani Fatma Amani… Read More
  • Dayna Nyange na Nay kunani?? Picha zanaswa, wenyewe wakana Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ akiwa katika pozi la nusu utupu na msanii wa Bongo Fleva, Aisha Nyange ‘Dayna’ Hii ni aibu yao! Picha zinazomuonesha staa wa Hip Hop anayetamba na ngoma ya Shika Adabu Yako, Emmanu… Read More
  • Wagombea warushiana matusi Marekani                      Wagombea wa urais nchini Marekani kupitia tiketi ya chama cha Republican Ted Crus na Donald Trump… Read More
  • Wanajeshi 8 mbaroni kwa mauaji    Askari nane wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), wanashikiliwa na Polisi Mkoa wa Kigona wakituhumiwa kwa mauaji ya Erick Nilamewa (16) waliyemtuhumu kuwaibia simu moja aina ya Techno na Sh. 6,000. Tuki… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE