July 04, 2014

chuji

AZAM FC: HATUJAINGIA MKATABA NA CHUJI, AMEOMBA KUFANYA MAZOEZI Kitaifa

chuji
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
BAADA ya taarifa kuenea mchana wa leo kuwa aliyekuwa kiungo mzoefu wa Yanga, Athumani `Idd Chuji` amesajiliwa na Azam kutokana na kuonekana katika mazoezi ya klabu hiyo kwenye uwanja wa Azam Complex, uongozi wa mabingwa hao umekanusha taarifa hizo.
Chuji aliyetemwa na Yanga alionekana katika jezi ya Azam fc, lakini  msemaji wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga  amesema klabu hiyo haijaingia mkataba wowote na kiungo huyo.
Jafar aliongeza kuwa Chuji aliomba kufanya mazoezi na Azam na kwasababu klabu hiyo inapenda michezo haikuona sababu ya kumnyima nafasi hiyo.
“Chuji aliomba kufanya mazoezi, uongozi ukaona si jambo la busara kumkatalia”. Alisema Jafar.
“Hata katika mazoezi ya leo jezi aliyovaa haikuwa na namba yoyote, kwahiyo hatuna mkataba wowote”.
Jafar alisisitiza kuwa jioni ya leo ameongea na katibu mkuu wa klabu hiyo, Nassor  Idrissa `Father` na alielezwa kuwa hakuna mkataba wowote ambao Azam fc imeingia na Chuji zaidi ya kuomba kufanya mazoezi.
‘Kuvaa jezi ya Azam sio kwamba ndio tumemsajili, sisi tunaenda kisasa. Tunapofanya mazoezi, timu moja inavaa jezi na timu nyingine inavaa jezi. Kama mchezaji yupo mazoezini lazima avae jezi, lakini hatuna mkataba na mchezaji huyo”.
Hata hivyo, Jafar alisema suala la Chuji kusajiliwa itategemeana na mwalimu atamuonaje katika mazoezi na kama ataonekana ana kiwango kizuri, kazi ya uongozi ni kutekeleza mahitaji ya mwalimu.
- See more at: http://shaffihdauda.com/?p=3036#sthash.uxAcf8RE.dpuf

  Na Baraka Mpenja, Dar es salaam 
BAADA ya taarifa kuenea kuwa aliyekuwa kiungo mzoefu wa Yanga, Athumani `Idd Chuji` amesajiliwa na Azam kutokana na kuonekana katika mazoezi ya klabu hiyo kwenye uwanja wa Azam Complex, uongozi wa mabingwa hao umekanusha taarifa hizo.  Chuji aliyetemwa na Yanga alionekana katika jezi ya Azam fc, lakini  msemaji wa klabu hiyo, Jafar Idd Maganga  amesema klabu hiyo haijaingia mkataba wowote na kiungo huyo.  Jafar aliongeza kuwa Chuji aliomba kufanya mazoezi na Azam na kwasababu klabu hiyo inapenda michezo haikuona sababu ya kumnyima nafasi hiyo.  “Chuji aliomba kufanya mazoezi, uongozi ukaona si jambo la busara kumkatalia”. Alisema Jafar.  “Hata katika mazoezi ya leo jezi aliyovaa haikuwa na namba yoyote, kwahiyo hatuna mkataba wowote”.  Jafar alisisitiza kuwa jioni ya leo ameongea na katibu mkuu wa klabu hiyo, Nassor  Idrissa `Father` na alielezwa kuwa hakuna mkataba wowote ambao Azam fc imeingia na Chuji zaidi ya kuomba kufanya mazoezi.  ‘Kuvaa jezi ya Azam sio kwamba ndio tumemsajili, sisi tunaenda kisasa. Tunapofanya mazoezi, timu moja inavaa jezi na timu nyingine inavaa jezi. Kama mchezaji yupo mazoezini lazima avae jezi, lakini hatuna mkataba na mchezaji huyo”.  Hata hivyo, Jafar alisema suala la Chuji kusajiliwa itategemeana na mwalimu atamuonaje katika mazoezi na kama ataonekana ana kiwango kizuri, kazi ya uongozi ni kutekeleza mahitaji ya mwalimu.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE