July 02, 2014

Zaidi ya vifo 450 vimetokana na Ebola huko Afrika Magharigi

Mawaziri wa afya 11 kutoka mataifa ya Afrika magharibi wanakutana mjini Accra, Ghana, kwa siku mbili ili kuzungumzia mkakati gani utumike kudhibiti kuenea kwa Ebola katika kanda hiyo.
Tayari visa vya ugonjwa huo vimepatikana katika nchi ya Guinea, Liberia na Sierra Leone, na shirika la afya duniani, WHO linasema kuwa hilo ndilo tukio kubwa zaidi la kusambaa kwa ugonjwa huo katika eneo kubwa.
Mkutano huo utazungumzia, tisho la hivi sasa la kuenea kwa ugonjwa huo.
Pia maelezo yatasikizwa kutoka kwa wagonjwa walionusurika, si tu kutoka Afrika magharibi, bali pia kutoka Uganda, taifa lililofaulu kupambana vilivyo na ugonjwa huo karibu miaka kumi iliyopita.
Viini vya ugonjwa hatari wa Ebola husambaa kwa kasi

Mkurupuko huo wa sasa tayari umewaua zaidi ya watu 450, wengi wao kutoka Guinea.
Mataifa mengine yanayotarajiwa kushiriki mkutano huo ni Ivory Coast, Mali, Guinea Bissau, Senegal, DRC na Gambia ambayo inasemekana kuwa katika hatari zaidi ya maambukizo hayo ya Ebola.
Ebola ni miongoni mwa magonjwa hatari sana duniani ambao hauna tiba kamilifu na vifo aghalabu hutokea muda mfupi baada ya maambukizo iwapo hamna mikakati kabambe ya kudhibiti athari zake kwa mgonjwa. Miongoni mwa athari hizo ni mgonjwa kuvuja damu na maambukizi hufanyika kwa kasi kutokana na majimaji ya mwilini ya mgonjwa kumpata mtu mwingine.
Katika hali hii ya sasa wataalam wanasema kuwa kuenea kwa ugonjwa huo kwatokana na unyanyapaa na uoga wa wagonjwa kutengwa huku visa vya wanafamilia kuwaficha wagonjwa wao vikiripotiwa.
Tayari Liberia na Sierra Leone wamonya kuwa yeyote atakayepatikana au kushukiwa kumficha mgonjwa wa Ebola, atashtakiwa.
Mikusanyiko na safari ya watu baina ya nchi pia kunatoa fursa kwa maradhi hayo kusambaa.
WHO tayari imewatuma wataalam zaidi ya 150, huko Afrika ya Magharibi, ili kusaidia kukabiliana na hali hiyo lakini wamesema kuwa utashi zaidi wa kisiasa unahitajika ili kupatikane suluhu la kudumu la kutokomeza kabisa ugonjwa huo.

Related Posts:

  • Yanga : "Kaseja Huru"   Ungozi wa klabu ya Yanga umesema hauna tatizo na golikipa Juma Kaseja endapo atataka kujiunga na timu nyingine yoyote ambayo ipo tayari kumsajili kwa ajili ya kuitumikia kwasababu kwa sasa mchezaji huyo hayupo k… Read More
  • Idadi ya wasanii waliotangaza kugombea Ubunge 2015 hii hapa Muigizaji Wema Sepetu ametangaza kuwania Ubunge wa viti maalum Singida Wasanii wa filamu na muziki wameamua kujitokeza kuwania nafasi za ubunge katika maeneo mbalimbali nchini katika uchaguzi wa 2015. Mpaka sasa… Read More
  • Nuh Mziwanda atimua kwa Shilole Mfungo wa mwezi Mtukufu wa Ramadhani umemfanya msanii wa Bongo Fleva,Nuh Mziwanda kuondoka nyumbani kwa mpenzi ambaye ni msanii,Shilole ili kumpisha mpenzi wake afunge kwani hawajafunga ndoa. Shilole ameyazungumza hay… Read More
  • Jicho letu October:Kwa nini Nyerere hana mrithi wa urais CCM ?   Ikiwa Tanzania inaeleke akatika tukio kubwa la ktaifa  Uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na rais, OCTOBER 2015. Hapa tunazidi kuwaletea Taarifa mbalimbali zinazohusiana na Uchaguzi mkuu.  Leo hii tuna… Read More
  • Wapinzani waipasua Serikali  Mwenyekiti wa maofisa watendaji wakuu wa makampuni, Ali Mufuruki (Kushoto) akiangalia kitabu cha Azimio la Tabora alilokabidhiwa na kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe (wa pili kushoto) baada ya kum… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE