July 21, 2014

 
Jaja akipokea nakala ya mkataba wake kutoka kwa Katibu Mkuu wa Young Africans, Bw. Beno Njovu leo mara baada ya kusaini kuitumikia kwa miaka miwili.
Hatimaye mshamabuliaji Geilson Santos Santana "Jaja"  raia wa Brazil leo amesaini mkataba wa miaka miwili (2014-2016) kuitumikia timu ya Young Africans kwa ajili ya michuano mbalimbali ikiwemo ya Ligi Kuu ya Vodacom pamoja na mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika mwakani.
Katibu mkuu wa Young Africans  Bw Beno Njovu amesema usajli wa Jaja unakua ni wa pili msimu huu kwa wachezaji wa kimataifa baada ya awali kumsajili kiungo mshambuliaji Andrey Coutinho ambaye pia ni raia wa Brazil.
"Kazi yetu uongozi ni kutekeleza maelekezo ya kocha mkuu pamoja na benchi la ufundi, walitoa mapendekezo ya usajili kabla hawajaanza kazi na mengine baada kuwasili yote tunajitahidi kuyatekeleza ili kila kitu kiende safi" alisema Beno.
Jaja ambaye alizaliwa tarehe 21 Septemba 1985 na kukulia katika mji wa Aracaju nchini Brazili mpaka anasajiliwa na timu ya Young Africans alikuwa akiichezea timu ya Itabaina FC iliyopo nchini Brazil.
Mshambuliaji huyo mwenye mwili uliojaa vizuri tayari alishaanza mazoezi tangu katikati ya wiki iliyopita chini ya Kocha Mkuu Marcio Maximo na msaidizi wake Leonado Neiva ambao wanaendelea kukinoa kikosi cha Young Africans kwa ajili ya michuano mbalimbali.
Picha na Young Africans

Related Posts:

  • Chenge, Ngeleja, Tibaijuka OutKamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi kimewasimamisha ujumbe wa Halmshauri Kuu ya chama hicho NEC wanachama wake watatu ambao ni wajumbe wa NEC kufuatia na kuhusika kwao katika sakata la akaunti ya Tegeta Escrow. Wajumbe hao ni m… Read More
  • Nisha afunguka uhusiano wake na Nay ndani ya Papaso    Msanii wa Filamu nchini, Salma Jabu maarufu Nisha, ameongea mambo mengi kuhusiana na sanaa yake, wasanii  na mahusinao yake ya kimapenzi na msanii Nay wa Mitego. Akizungumza na D'Jaro Alungu ndani ya Pap… Read More
  • Msiba:Kapten John Komba amefariki dunia    Mbunge wa Mbinga  Mh: john Komba, amefariki Dunia jioni hii. Taarifa za kifo cheke zimetolewa katika A/C ya Twitter ya CCM na kusambaa katika vyombo mbalimbali .    Kepteni Komba enzi za uha… Read More
  • Pole Chris Brown mwenzako nilichekwa-Ommy Dimpoz    Msanii Omary Nyembo alimaarufu kama Ommy Dimpoz amefunguka na kusema kuwa watu wa uhamiaji duniani kote huwa hawatambui umaarufu wa mtu pindi wanapogundua kuna kitu hakijaenda sawa,Ommy Dimpoz amefunguka hay… Read More
  • Diamond atajwa kuwania tuzo nyinge kubwa Africa Diamond Platnumz ametajwa kuwania tuzo za 16 za Vodafone Ghana Music (Awards), VGMA 2015. Majina ya wasanii watakaowania tuzo hizo yametajwa kwenye hoteli ya La Palm Royal Beach Hotel jijini Accra, jana Ijumaa, Februar… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE