Fabio
Borini, 23, anajiandaa kujiunga na Sunderland baada ya Liverpool
kukubali ada ya pauni milioni 14 (Sky Sports), baada ya kumchukua Filipe
Luis siku ya Ijumaa, Chelsea wanazungumza na Atlètico Madrid kuhusu
kumsajili beki kutoka Brazil Joao Miranda, 29 kwa pauni milioni 20
(Daily Star), Real Madrid wanafikiria kumchukua Alvaro Negredo, 28,
kutoka Manchester City kuziba nafasi ya Alvaro Morata, 20, anayekwenda
Juventus (Metro), Liverpool wamemwambia Loic
Remy, 27 kupunguza madai ya mshahara mkubwa kama anataka kufanikisha
uhamisho wake wa pauni milioni 8 kutoka QPR (Daily Mirror), QPR wamepewa
nafasi ya kumsajili Samuel Eto'o lakini huenda wakakataa kutokana na
kutokubaliana mshahara (Daily Mail), Arsenal watakabiliwa na ushindani
kutoka Valencia kumsajili kipa David Ospina, 25 (Metro), Everton
wanakaribia kufikia makubaliano ya kumsajili Romelu Lukaku, 21, kutoka
Chelsea kwa uhamisho wa kudumu (Daily Mail), Tottenham wanakaribia
kukamilisha uhamisho wa pauni milioni 10 wa beki Ben Davies, 21, kutoka
Swansea. Liverpool pia walikuwa wakimtaka (Daily Telegraph), boss wa
QPR, Harry Redknapp amesema anapanga kusajili wachezaji "sita au saba"
zaidi kabla ya kuanza msimu mpya (Times), AC Milan wapo tayari kusubiri
mwisho wa dirisha la usajili kuanza kumfuatilia Nani ambaye Manchester
United wanataka euro milioni 14 (Corriere dello Sport).
July 19, 2014
7:13 AM
Machaku
No comments
Related Posts:
Yanga VS Mazembe, Kiingilio bure Klabu ya Yanga imeamua kutoa fursa kwa mashabi wake na mashabiki wa soka la Tanzania kuingia bure kwenye mchezo wao wa kombe la shirikisho Afrika dhidi ya TP Mazembe miamba ya soka la DR Congo mchezo unaotarajiwa kuc… Read More
Wananchi Watinga Mahakamani Kufungua Kesi ya Kupinga Agizo la Serikali Kuzuia Matangazo ya Moja kwa Moja ya Bunge HATUA ya serikali kuzuia kurusha moja kwa moja mjadala wa vikao vya Bunge kama ilivyokuwa awali, bado inaumiza wananchi. Safari hii wananchi wametinga mahakamani na kwamba leo wamefika katika Mahakama… Read More
Kurasa za Magazetini leo hii jumatatu 27 june 2016 Habari mpenzi msomaji. Karibu katika kurasa za magazetini leo hii ikiwa ni Jumatatu ya 27 june 2016 sawa na ramadhani 22.Habari zote kubwa zipo hapa … Read More
News: Rais Magufuli afanya mabadiliko wakuu wa Mikoa na kuteua wakuu wa Wilaya 139 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139. Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Joh… Read More
Huu ndiyo utajiri wa Diamond Kumekuwepo na tetesi nyingi kuhusu utajiri wa Diamond umefikia kiasi gani. Hilo ni swali ambalo hajawahi kulijibu kwa uhakika zaidi ya kutoa tu hints na kuwaacha wanaouliza kubaki na majibu yao wenyewe vichwani.Lakini… Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 MAONI YAKO:
Post a Comment