Fabio
Borini, 23, anajiandaa kujiunga na Sunderland baada ya Liverpool
kukubali ada ya pauni milioni 14 (Sky Sports), baada ya kumchukua Filipe
Luis siku ya Ijumaa, Chelsea wanazungumza na Atlètico Madrid kuhusu
kumsajili beki kutoka Brazil Joao Miranda, 29 kwa pauni milioni 20
(Daily Star), Real Madrid wanafikiria kumchukua Alvaro Negredo, 28,
kutoka Manchester City kuziba nafasi ya Alvaro Morata, 20, anayekwenda
Juventus (Metro), Liverpool wamemwambia Loic
Remy, 27 kupunguza madai ya mshahara mkubwa kama anataka kufanikisha
uhamisho wake wa pauni milioni 8 kutoka QPR (Daily Mirror), QPR wamepewa
nafasi ya kumsajili Samuel Eto'o lakini huenda wakakataa kutokana na
kutokubaliana mshahara (Daily Mail), Arsenal watakabiliwa na ushindani
kutoka Valencia kumsajili kipa David Ospina, 25 (Metro), Everton
wanakaribia kufikia makubaliano ya kumsajili Romelu Lukaku, 21, kutoka
Chelsea kwa uhamisho wa kudumu (Daily Mail), Tottenham wanakaribia
kukamilisha uhamisho wa pauni milioni 10 wa beki Ben Davies, 21, kutoka
Swansea. Liverpool pia walikuwa wakimtaka (Daily Telegraph), boss wa
QPR, Harry Redknapp amesema anapanga kusajili wachezaji "sita au saba"
zaidi kabla ya kuanza msimu mpya (Times), AC Milan wapo tayari kusubiri
mwisho wa dirisha la usajili kuanza kumfuatilia Nani ambaye Manchester
United wanataka euro milioni 14 (Corriere dello Sport).
July 19, 2014
7:13 AM
Machaku
No comments
Related Posts:
Ni Clouds FM tena, yapata tuzo ya Super Brand Radio Afrika Mashariki Kwa mara nyingine Clouds Fm imepokea tuzo bora za viwango ‘Super Brand’’ 2015-2016. Mkuu wa Kitengo cha Idara ya uchambuzi wa viwango Afrika Mashariki,Jawad Jaffer akizungumza wakati akitoa t… Read More
Nani zaidi kati ya Mayweather Vs Pacquiao? Kitendawili hiki, jibu lake laja hivi punde Japo tayari ni tajiri ,Mayweather ambae jina lake la utani ni Money, inatarajiwa atapokea zaidi ya dolla millioni $150m na Pacquiao kama millioni $100m. … Read More
Brand new song -Young Killer ft Ommy Dimpoz, ROMA na Lina - Mungu baba Young Killer Msodoki anakuletea collabo ya mwaka akiwashirikisha Ommy Dimpoz, ROMA na Lina. Wimbo unaitwa MUNGU BABA.Hutakiwi kukosa kabisa kuskia kilichofanyika humu ndani. Download hapa chini … Read More
List kamili ya waliopendekezwa kushiriki Kili Music Awards 2014-2015 1. MTUMBUIZAJI BORA WA MUZIKI WA MWAKA- KIUME 1 MZEE YUSSUF 2 CHRISTIAN BELLA 3 DIAMOND PLANUMZ 4 ALLY KIBA 5 NYOSHI EL SAADAT 2.MTUMBUIZAJI BORA WA MUZIKI WA MWAKA- KIKE 1 VANESSA MDEE 2 KHADIJA KOPA 3 ISHA MASHAUZI… Read More
Zari All White Party 2015 ni nomaaa, haijwahi kutokea, mambo 3 makubwa ni haya Zari na Diamond wakiingia ukumbini Diamond akitoa burudani Maliki wa mipasho nchini bi Hadija Kopa naye alikuwepo Swahiba mkubwa wa Diamond Shetta akifanya yake Diamond … Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 MAONI YAKO:
Post a Comment