Padri Miguel enzi za uhai wake.
PADRI raia wa Hispania, Miguel Pajares, 75, aliyeambukizwa virusi vya
Ebola wakati akifanya kazi Afrika Magharibi amefariki dunia akiwa
hospitalini mjini Madrid.Padri Miguel alikuwa anafanya kazi katika Hospitali ya Mtakatifu Joseph iliyopo mjini Monrovia, Liberia.
Alisafirishwa kwenda Hispania kutoka Liberia wiki iliyopita akiwa na mtawa mmoja ambaye naye aliponea chupuchupu kuambukizwa homa hiyo.
Zaidi ya watu 1,000 wamefariki kutokana na homa ya Ebola nchini Liberia, Guinea, Sierra Leone na Nigeria tangu kulipuka kwa homa hiyo mwezi…
0 MAONI YAKO:
Post a Comment