October 25, 2014

Iran Madam 
Reyhaneh Jabbari mwenye umri wa miaka 26 amehukumiwa kunyongwa baada ya kukutwa na hatia ya kumuua mtu mmoja ambaye alifanya jaribio la kumbaka.
Taarifa iliyoripotiwa na CNN inasema mwanamke huyo amenyongwa katika gereza la Tehrain, Iran ambapo alikuwa amefungwa baada ya kutenda kosa hilo mwaka 2007 wakati huo akiwa na umri wa miaka 19.
Mwanamke huyo amekutwa na hatia hiyo kutokana na kosa la kumuua aliyekuwa mfanyakazi wa wizara ya ulinzi na usalama nchini Iran, Morteza Abdolali.
Shirika la kimataifa la haki za binadamu Amnesty International limelaani kitendo cha Iran kutoa hukumu hiyo, ambapo mbali na jitihada ya kampeni mbali mbali zilizofanywa ikiwemo zile za kwenye mitandao ya kijamii katika kuipinga hukumu hiyo kuonekana kutozaa matunda.
Taarifa kutoka nchini humo zinasema mahakama ilitoa hukumu hiyo baada ya kutojiridhisha na utetezi alioutoa mahakamani kwamba alitenda kosa hilo akiwa anajilinda.
Utafiti wa Umoja wa Mataifa wa mwaka 2011 unaonesha Iran ni moja ya nchi zinazoongoza kwa ukiukwaji wa haki za binadamu ambapo nchi hiyo ina wastani wa kutoa hukumu ya kunyongwa mtu 1 kila baada ya masaa 8.

Related Posts:

  • Wachunguzi waanza kuchunguza chanzo cha motoMaafisa wanasema moto ulianza ghorofa ya 20 upande wa nje na haukusambaa ndani ya hoteli Wachunguzi mjini Dubai wanajaribu kubaini chanzo cha moto uliozuka katika hoteli ya kifahari mkesha wa Mwaka Mpya na kujeruhi watu kadha… Read More
  • Magazeti ya leo January 1 -2016 haya hapa Leo January1 2016, tukiwa tunasherehekea siku ya mwaka mpya, tunakuletea kilichoandikwa katika magazeti ya leo japo kwa ufupi … Read More
  • CUF kususia maadhimisho ya mapinduzi Chama cha Wananchi kimesema hakitashiriki maadhimisho ya Sherehe za Mapinduzi visiwani Zanzibar kutokana na utata kuhusu matokeo ya uchaguzi. Chama hicho kupitia taarifa kimesema maadhimisho hayo yatafanyika “Serikali ik… Read More
  • Vigodoro, baikoko marufuku BARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), limeanza kung’ata kwa kutumia kanuni ili kudhibiti uchafuzi wa mazingira kwa kelele na mitetemo. Kwa sasa mtu akitaka kufanya sherehe mtaani, kupiga muziki k… Read More
  • KATY PERRY TO JOHN MAYER YOU MAKE ME FEEL LIKE A NATURAL WOMAN   John Mayer and Katy Perry partied like 18-year-old's ... clubbing till 4:30 AM Thursday, and that's after John raged on stage at a concert earlier in the day with the Grateful Dead. Check out the cli… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE