Mtangazaji
Maimartha Jesse na staa wa Bongo Fleva,Chege Chigunda wameingia kwenye
bifu baada ya mtangazaji huyo kupost picha mtandaoni ikimuonyesha Chege
akiwa jukwaani huku amefunga kitambaa cheusi mkononi na kuandika
….Angalia mkono Wa kushoto Wa chegge @chegechigunda hiiii ni hirizi ?
any way isiwe kesi jiachie chege ila mziki mziki wako naupenda hata
ukiniroga saw a Tu...japo cna imani hiyoo .
Akizungumza kwenye Uheard na Soudy Brown Chege alisema kuwa amemshangaa
sana mtangazaji huyo baada ya kupost picha hiyo na kusema kuwa hiyo siyo
hirizi bali ni kitambaa cheusi ambacho alikivaa alipokuwa kwenye shoo
mkoani Dodoma lengo ni kumuenzi msanii mwenzake Mez B aliyefariki dunia
wiki iliyopita mjini humo. ‘’Jamani hiyo siyo hirizi na huwezi kuvaa
hirizi mchana kile kilikuwa ni kitambaa cheusi lengo lilikuwa ni
kumuenzi Mez B,’alisema Chege.
Naye Maimartha Jesse akizungumzia suala hilo alisema kuwa hakuwa na nia mbaya ndiyo maana aliuliza ili watu wamwambie ni kitu gani amevaa Chege na mwisho alimuomba msamaha Chege baada ya kumkwaza kwa tukio hilo.
Naye Maimartha Jesse akizungumzia suala hilo alisema kuwa hakuwa na nia mbaya ndiyo maana aliuliza ili watu wamwambie ni kitu gani amevaa Chege na mwisho alimuomba msamaha Chege baada ya kumkwaza kwa tukio hilo.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment