March 17, 2015

 
Spika wa Bunge Mh Anne Makinda amesema kuwa kwa niaba ya Bunge bado anamtambua mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kuwa ni mbunge halali wa bunge hilo.
Akizungumza nje ya ukumbi wa bunge mara baada ya kikao cha Bunge kumalizika leo majira ya saa 5 Asubuhi, Makinda amesema kuwa anasubiri barua rasmi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ambayo ndiyo itakayompa mwongozo kuhusu ubunge wa Zitto Kabwe.
Amesema kwa mujibu wa taratibu, kama chama kikimvua uanachama mbunge, kinapaswa kuiandikia Tume ya Taifa ya Uchaguzi, ambayo nayo inatoa mwongozo kwa bunge, jambo ambalo halijafanyika hadi sasa.
Kwa upande wake Mwanasheria Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Mh. Tundu Lissu alipoulizwa kuhusu suala hilo amesema kuwa anayetakiwa kuandika barua hiyo ni Katibu Mkuu wa Chama, na si yeye na kwamba hajapata taarifa kama barua hiyo imeandikwa au la..!

Related Posts:

  • Breaking News: Misanya Bingi afariki Dunia   Aliyewahi kuwa mtangazaji maarufu sana wa Radio nchini kupitia Radio One Stereo na ITV Dkt. Misanya Dismas Bingi maarufu Misanya Bingi amefariki Dunia. Taarifa za awali zinasema, misanya Bingi amefariki Dunia usiku … Read More
  • Kiswahili kuwa Lugha rasmi ya Afrika Kiongozi wa chama cha watetezi wa Uhuru wa kiuchumi (EFF) cha Afrika Kusini, Julius Malema, ametoa wito wa kupitishwa kwa lugha moja itakayotumika barani Afrika, huku akipendekeza lugha ya Kiswahili kuwa lugha hiyo. Ma… Read More
  • Luka Modric Anyakua Mchezaji Bora, Ronaldo Mshambuliaji Bora KIUNGO wa Klabu ya Real Madrid na nahodha wa timu ya taifa ya Croatia, Luka Modric amefanikiwa kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa Ulaya akiwafunika Mo Salah wa Liverpool na Cristiano Ronaldo wa Juventus. DATA 17/18 … Read More
  • Sakata la Makontena ya Makonda,Musiba amkaanga   Lile sakata la makontena ya Bandarini yanayohusishwa na mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Poul Makonda, hatimaye linazidi kuchukua sura mpya baada ya leo Mkurugenzi wa CZI Cyprian Musiba kuifunguka kila kitu na kumuw… Read More
  • KUTOKA IKULU:Taarifa kwa vyombo vya Habari   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewataka viongozi wote nchini kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria sambamba na kuhakikisha wanasimamia ipasavyo matumizi ya rasilim… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE