Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza kuwa, Watanzania
wengine 20 waliolazimika kuyakimbia makazi yao huko Johannesburg nchini
Afrika Kusini wako salama na wiki hii wanatarajiwa kurejeshwa nyumbani
baada ya kuibuka wimbi la hujuma na mashambulio dhidi ya wageni nchini
humo. Kundi la kwanza la Watanzania 26 wanaoishi nchini Afrika Kusini
lilirejea nyumbani Jumamosi iliyopita baada ya kushadidi hujuma na
mashambulio dhidi ya wageni. Mkuu wa Mawasiliano katika Wizara ya Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mindi Kasiga amesema kwamba,
serikali inakamilisha utataribu wa kuwatambua Watanzania wengine 20
waliobakia ambao watarejeshwa nyumbani. Amesema kuna haja ya kuhakikisha
uraia wao kuna kuna wengi ambao wanadai kuwa ni Watanzania na
wanazungumza vizuri Kiswahili lakini kiuhakika sio raia wa Tanzania.
Wakati huo huo, habari kutoka nchini Afrika Kusini zinasema kuwa, hali
ya mambo nchini humo imeanza kurejea katika hali yake ya kawaida baada
ya majuma kadhaa ya hujuma na mashambulio dhidi ya raia wa kigeni.
WAKILI KISABO AWASILISHA MADA KUHUSU MCHANGO WA THRDC KWA WAANDISHI WA
HABARI NCHINI
-
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umeshiriki katika
kongamano la wadau wa habari nchini Tanzania lililoendeshwa na
MISA-Tanzania kat...
8 hours ago
0 MAONI YAKO:
Post a Comment