Makamu wa Rais nchini Iraq amesema kuwa baadhi ya nchi katika eneo la
Mashariki ya Kati zinaendesha sera zenye lengo la kuivuruga na kuigawa
nchi yake. Nouri al-Maliki amesema, mipango yoyote ya kuigawa Iraq
itakabiliwa na upinzani wa kila kona kutoka kwa wananchi ambao siku zote
wamesimama kidete kutetea umoja wa taifa lao. Hii ni katika hali
ambayo, baadhi ya nchi za Kiarabu zinashirikiana na Marekani kuigawa
Iraq katika majimbo matatu. Muswada uliowasilishwa kwenye Congress ya
Marekani unataka Iraq igawanywe mara tatu na wapiganaji wa Kikurdi
waweze kupewa silaha moja kwa moja kutoka Washington bila ridhaa ya
Baghdad. Kiongozi wa Kishia nchini Iraq, Muqtada al-Sadr ameionya
Congress dhidi ya kupitisha muswada huo. Nouri al-Maliki, makamu wa rais
wa Iraq amesema muswada huo una mkono wa baadhi ya nchi za Kiarabu za
Mashariki ya Kati.
MRADI WA TAZA MBIONI KUKAMILIKA - KAPINGA
-
📌 Unahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka Iringa hadi
Sumbawanga
📌 Kapinga asema Mkoa wa Rukwa kuunganishwa na gridi ya Taifa kupitia mrad...
4 hours ago
0 MAONI YAKO:
Post a Comment