Makamu wa Rais nchini Iraq amesema kuwa baadhi ya nchi katika eneo la
Mashariki ya Kati zinaendesha sera zenye lengo la kuivuruga na kuigawa
nchi yake. Nouri al-Maliki amesema, mipango yoyote ya kuigawa Iraq
itakabiliwa na upinzani wa kila kona kutoka kwa wananchi ambao siku zote
wamesimama kidete kutetea umoja wa taifa lao. Hii ni katika hali
ambayo, baadhi ya nchi za Kiarabu zinashirikiana na Marekani kuigawa
Iraq katika majimbo matatu. Muswada uliowasilishwa kwenye Congress ya
Marekani unataka Iraq igawanywe mara tatu na wapiganaji wa Kikurdi
waweze kupewa silaha moja kwa moja kutoka Washington bila ridhaa ya
Baghdad. Kiongozi wa Kishia nchini Iraq, Muqtada al-Sadr ameionya
Congress dhidi ya kupitisha muswada huo. Nouri al-Maliki, makamu wa rais
wa Iraq amesema muswada huo una mkono wa baadhi ya nchi za Kiarabu za
Mashariki ya Kati.
May 17, 2015
7:15 AM
Machaku
No comments
Related Posts:
Video: Maagizo ya Magufuli kwa wanaolipwa mishahara hewa March 15 2016 wakuu wapya wa mikoa nchini walikuwa wakiapisha Ikulu, Dar es salaam. Licha ya kuwa ndio kwanza wamepewa viapo, lakini Rais John Pombe Magufuli amewaagiza wakuu hao wa Mikoa kuhakikisha ndani … Read More
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), David Mattaka Ashitakiwa Tena Kwa Uhujumu Uchumi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), David Mattaka, amepandishwa kizimbani kwa kosa la kuliingizia serikali hasara ya Dola za Marekani 772,402.08. Akisoma mashtaka hayo jana, Vitalis Thimo… Read More
Magazeti ya leo jumatano 16 march 2016 haya hapa Karibu mpendwa wa ubalozini.blogspot.com katika kurasa za magazeti ya leo. Makubwa yaliyondikwa ni haya hapa … Read More
Majimbo 5 kuwateua wagombea urais Marekani Majimbo matano nchini Marekani yanapiga kura kumteua mgombea atakayewania urais kupitia tiketi ya vyama vyao. Uchaguzi huo huenda ukawapa fursa wagombea wa vyama vya Democrat na Republican kuimarisha uongozi… Read More
Messi kavunja rekodi nyingi FC Barcelona Mshambuliaji wa kimataifa wa Argentina anayeichezea klabu ya FC Barcelona ya Hispania Lionel Messi ameweka na kuvunja rekodi nyingi akiwa ndani ya klabu ya FC Barcelona ya Hispania, ila March 15 101greatgoals.co… Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 MAONI YAKO:
Post a Comment