Makamu wa Rais nchini Iraq amesema kuwa baadhi ya nchi katika eneo la
Mashariki ya Kati zinaendesha sera zenye lengo la kuivuruga na kuigawa
nchi yake. Nouri al-Maliki amesema, mipango yoyote ya kuigawa Iraq
itakabiliwa na upinzani wa kila kona kutoka kwa wananchi ambao siku zote
wamesimama kidete kutetea umoja wa taifa lao. Hii ni katika hali
ambayo, baadhi ya nchi za Kiarabu zinashirikiana na Marekani kuigawa
Iraq katika majimbo matatu. Muswada uliowasilishwa kwenye Congress ya
Marekani unataka Iraq igawanywe mara tatu na wapiganaji wa Kikurdi
waweze kupewa silaha moja kwa moja kutoka Washington bila ridhaa ya
Baghdad. Kiongozi wa Kishia nchini Iraq, Muqtada al-Sadr ameionya
Congress dhidi ya kupitisha muswada huo. Nouri al-Maliki, makamu wa rais
wa Iraq amesema muswada huo una mkono wa baadhi ya nchi za Kiarabu za
Mashariki ya Kati.
May 17, 2015
7:15 AM
Machaku
No comments
Related Posts:
Kurasa za magazetini leo hii Jumamosi ya 17 Desember 2016 Habari mpenzi msomaji. Karibu katika kurasa za magazetini leo hii Jumamosi ya 17 Desember 2016. Habari kbwa zilizobeba uzito wa juu ni pamoja a hizi &nbs… Read More
Mlithi wa Malecela wa NIMR huyu hapa Siku moja tu baada ya rais wa Jamhuri ya Muungano nwa Tanzania Dokta John Magufuli, kutengua uteuzi wa aliyekuwa Mkurugenzi mkuu wa Taifa bwa taasisi ya utafiti wa magonjwa ya Binadam NIMR, hatimaye rais Magufuli … Read More
BREAKING NEWS:Rais Magufuli atengua uteuzi wa Mkurugenzi mkuu wa Taifa wa utafiti wa Magonjwa nya Binadam Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania DK. JohN Pombe Magufuli, ametengua uteuzi wa aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa taasisi ya utafiti wa magonjwa ya Binadamu -NIMR Dokta Mwele Malecela. Uteuzi wa kujaza nafas… Read More
Wyre kutoka nchini Kenya ametuletea video hii mpya Wyre has a new music video out #wyreworkandplay Kevin Waire better known as Wyre Da Love Child is a Kenyan R&B and reggae musician from known from the some of the most popular groups in musi… Read More
Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili ya Disemba 18 Habari mpenzi wa Machaku Media. Karibu katika kurasa za Magazetini leo hii Jumapili ya 18 December 2016. Tumekusogezea hapo ulipo uweze kupitia kurasa za mbele na za nyuma katika magazeti yetu le… Read More
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 MAONI YAKO:
Post a Comment