Makamu wa Rais nchini Iraq amesema kuwa baadhi ya nchi katika eneo la
Mashariki ya Kati zinaendesha sera zenye lengo la kuivuruga na kuigawa
nchi yake. Nouri al-Maliki amesema, mipango yoyote ya kuigawa Iraq
itakabiliwa na upinzani wa kila kona kutoka kwa wananchi ambao siku zote
wamesimama kidete kutetea umoja wa taifa lao. Hii ni katika hali
ambayo, baadhi ya nchi za Kiarabu zinashirikiana na Marekani kuigawa
Iraq katika majimbo matatu. Muswada uliowasilishwa kwenye Congress ya
Marekani unataka Iraq igawanywe mara tatu na wapiganaji wa Kikurdi
waweze kupewa silaha moja kwa moja kutoka Washington bila ridhaa ya
Baghdad. Kiongozi wa Kishia nchini Iraq, Muqtada al-Sadr ameionya
Congress dhidi ya kupitisha muswada huo. Nouri al-Maliki, makamu wa rais
wa Iraq amesema muswada huo una mkono wa baadhi ya nchi za Kiarabu za
Mashariki ya Kati.
SOUWASA YAPITA NYUMBA KWA NYUMBA KUHAMASISHA WATEJA KUREJESHA HUDUMA ZA MAJI
-
Wafanyakazi wa SOUWASA wakitoa elimu kwa mwananchi na mkazi wa Ruhuwiko
Shuleni kuhusu umuhimu wa matumizi ya maji na kutumia fursa iliyotolewa
bure ya ku...
9 hours ago
0 MAONI YAKO:
Post a Comment