May 20, 2015

Watanzania watakiwa kudumisha amani na utulivu 
Viongozi wa dini, wanasiasa na wazee nchini wamewaonya Watanzania kujiepusha na viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani. Viongozi hao walisema hayo, Dar es Salaam jana katika Mkutano kuhusu Amani na Utulivu wa Tanzania, ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere. Akizungumza katika mkutano huo, Mwenyekiti wa Bodi ya taasisi hiyo, Dk Salim Ahmed Salim, alisema ni wakati sasa wa Watanzania kuanza kuchukua hatua za kulinda amani iliyodumu kwa muda mrefu na kuipatia sifa ndani na nje ya nchi. Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba alisema tayari taifa la Tanzania limeanza kuwa na viashiria hatari vya uvunjifu wa amani, hali inayolazimu kuchukuliwa hatua za haraka ili kuhamasisha umoja na mshikamano. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, alitaja viashiria vilivyoanza kuonekana nchini vya uvunjifu wa amani kuwa ni mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), wazee na vikongwe, migogoro ya kisiasa, ardhi, wakulima na wawekezaji, kutoaminiana na kutotendewa haki sawa. Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba, alisema msingi wa amani siku zote ni kuwepo kwa haki, endapo haki itakosekana lazima kutakuwepo na tatizo la amani.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE