June 20, 2015

 
BILA kuwataja kwa majina, msanii wa filamu Bongo, Ruth Suka ‘Mainda’ amesema kitendo cha baadhi ya wasanii wanaojiona wamefikia vilele vyote vya mafanikio na kuwafanyia roho mbaya wenzao, ndiyo moja kati ya sababu kubwa zinazochangia sanaa ya uigizaji kuporomoka. Akibwabwaja’ na mwandishi wetu hivi karibuni, Mainda ambaye kwa sasa ‘amepangua gia’ zote zenye kasi katika sanaa na kuamua kujikabidhi madhabahuni kwa Mungu, alisema wasanii wasihangaike kumtafuta mchawi, badala yake wajichunguze na kujitazama upya kwani wengi wao wana roho mbaya za kutotaka wengine wapige hatua katika sanaa.
“Hakuna watu wenye roho mbaya kama wasanii wa uigizaji, kuna ambao wanajiona wamefika vilele vya mafanikio na  kwamba hakuna mwingine zaidi yao, hivyo wamekuwa wakiwafanyia fitina wanaokuja kwa kasi kwa kuwapiga majungu, wajiangalie upya na Mungu wa mbinguni awasaidie sana,” alisema Mainda.

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE