August 22, 2015

Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye ametangaza rasmi kujiondoa kutoka Chama cha Mapinduzi CCM na kujiunga na UKAWA.
Sumaye anakuwa Waziri Mkuu Mstaafu wa pili kujiunga na UKAWA baada ya Mhe. Edward Lowassa kufanya hivyo.
 
 Sumaye akiongea na vyombo vya habarileo mchana
Sumaye amejiunga rasmi na Ukawa wakati wa mkutano wa wanahabari na viongozi wa Umoja huo,  mkutano uliofanyika mchana wa leo katika ukumbi wa hoteli ya Kunduchi jijini Dar.
Aidha Sumaye hakusema ni chama gani amejiunga nacho, licha ya kubainisha lengo lake kuu la kuondoka CCM ni kwenda kuimarisha Ukawa na kuongeza nguvu kwenye vyama vya upinzani hasa katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 25.

Related Posts:

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE