September 18, 2015

Saudia inabeba dhima ya ajali ya winchi Makka 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Saudi Arabia inabeba dhima ya ajali ya hivi karibuni ya winchi au kreni katika Masjidul Haram Makka ambapo mahujaji zaidi ya 107 walipoteza maisha. Hussein Amir Abdulahian, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema uzembe wa wakuu wa Saudi Arabia na kutozingatiwa kanuni za usalama ndio chanzo kikuu cha ajali ya Makka ambayo pia lilipelekea zaidi ya watu 230 kujeruhiwa. Uchunguzi kuhusu ajali hiyo ya Ijumaa iliyopita Makka umebaini kuwa kulikuwa na kosa la kiufundi katika winchi iliyowaangukia mahujaji na wala si upepo mkali kama ilivyodaiwa. Shirika la Binladin lenye kandarasi ya kupanua Masjidul Haram limelaumiwa kwa kutozingatia sheria za ujenzi katika kazi zake. Huku hayo yakijiri, Alkhamisi ya jana kuliibuka moto mkubwa katika hoteli moja ya mahujaji mjini Makka ambao watu wawili walijeruhiwa huku watu wote zaidi ya 1000 waliokuwa ndani ya hoteli hiyo wakiondolewa mara moja ili kuepusha maafa. 

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE