September 18, 2015

 
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Profesa Patrick Makungu akifafanua jambo
Wamiliki wa mitandao ya mawasiliano nchini wametakiwa kutoa taarifa haraka juu ya makosa ya uharifu wa mitandaoni pindi yanapojitokeza, ili kuvirahisishia vyombo vya usalama kuweza kuchukua hatua za haraka kwa wahusika.
 
Wito huo umetolewa leo mkoani Mtwara na mkuu wa upelelezi wa polisi wilaya ya Masasi, SP Nathaniel Kyando, wakati wa semina ya mahakimu, waendesha mashitaka na wapelelezi kuhusu elimu ya sheria ya makosa ya mtandao na sheria ya miamala ya kielektroniki ya mwaka 2015.
Kwa upande wake, mkuu wa kitengo cha sheria kutoka Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Veronica Sudayi, akizungumza kwa niaba ya katibu mkuu wa wizara hiyo, amesema jamii inatakiwa kufahamu kwamba sheria hiyo haina vitu vipya isipokuwa ni mabadiliko ya kimfumo ambayo yameingiza makosa hayo katika mfumo wa kielektroniki.
Aidha, mwanasheria kutoka wizara hiyo, Anna Kalamo, amesema miongoni mwa mada ambazo wanapatiwa wahusika ni pamoja na sheria mbili ambazo zimepitishwa na serikali za miamala ya kielektroniki na sheria ya makosa ya mitandao zote za mwaka 2015 ambazo zimetungwa kwa lengo la kuleta ulinzi na matumizi salama ya mitandao hapa nchini.

Related Posts:

  • MSIBA: G_ STAR WA UKWELI AMEFARIKI DUNIA    Taarifa toka kwa watu wa karibu na marehemu pamoja na familia, imethibitisha kifo cha mdau mkubwa asana wa media Tanzania G_ STAR wa ukweli. Tratibu za mazishi zinafanyika na marehemu atazikwa siku ya Jumatat… Read More
  • AUDIO// KWA AJILI YAKO- PROFESSOR JAY fy CHAMELEONE   Mkali wa muziki wa  Rap toka nchini Tanzania Professor Jay Mwana lizombe, ameachia ngoma yake mpya kabisa aliyomshirikisha mkali wa muziki toka uganda Josee Chameleone. DOWNLOAD HAPA CHINI … Read More
  • PUMZIKA KWA AMANI AISHA MADINADA ALIYEKUWA mnenguaji na mwimbaji wa Bendi ya Twanga Pepeta, Aisha Madinda amefariki dunia mchana wa leo katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa ASET, Asha Baraka amethibitisha kutokea kifo hi… Read More
  • WABUNGE WAZICHAPA KAVU KAVU MJENGONI Seneta Johnston Muthama aliyejeruhiwa mguuni na kuchaniwa suruali yake wakati wa vurugu bungeni leo. WABUNGE nchini Kenya leo wametofautiana bungeni na kuamua kutupiana makonde huku wengine wakichaniana nguo kufuatia mjad… Read More
  • MAZISHI YA AISHA MADINDA YA AHIRISHWA   Aisha Madinda - enzi za uhai wake alipokuwa stejini. ALIYEKUWA mnenguaji na mwimbaji wa Bendi ya Twanga Pepeta, Aisha Madinda aliyefariki jana asubuhi, atazikwa kesho mchana badala ya leo kama ilivyokuwa imepangwa… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE