September 18, 2015

Daniel Amokachi
Amokachi alikuwa ameeleza hamu yake ya kutaka kushinda vikombe akiwa na FC IfeanyiUbah
Nahodha wa zamani wa Nigeria Daniel Amokachi amejiuzulu wadhifa wake kama meneja wa kilabu ya ligi kuu ya Nigeria FC IfeanyiUbah baada ya kuhudumu wiki tano pekee.
Mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 42 alikuwa awali ameeleza hamu yake ya kutaka kushinda vikombe na kuhakikisha kilabu hiyo inafana.
Lakini ameamua kuondoka baada ya msururu wa matokeo mabaya na kutoelewana kati yake na mmiliki wa kilabu hiyo.
“Nasikitika kuondoka baada ya kipindi kifupi hivi lakini kandanda inaendelea,” Amokachi ameambia BBC.
"Nilikuwa shabiki wa kilabu hii kabla ya kuteuliwa kwangu kama meneja kwa sababu ya msingi uliopelekea kuundwa kwake.
"Lakini sasa naitakia kila la heri na nitafuatilia hatua wanazopiga kwa fahari kuu.”
Ripoti zimedokeza kuwa Amokachi hakufurahishwa na sera ya klabu hiyo ya kutumia barabara hatari usiku kurejea nyumbani baada ya kucheza mechi za ugenini.
Msimamo wake ulimfanya kukosana na milionea anayemiliki klabu hiyo, Ifeanyi Ubah.
Mfanyabiashara huyo anaaminika kuchukulia hatua ya kocha huyo kuwa kukaidi mamlaka yake.
Amokachi alikataa kusema lolote alipoulizwa kuhusu suala hilo.
“Soka haitabiriki na hakuna wakati wa kwenda mbele na nyuma,” alisema.
"Imekuwa heshima kubwa kuhusika katika kilabu hii lakini kwa sasa safari yangu imefikia kikomo FC IfeanyiUbah."

Related Posts:

  • Mwamuzi wa Chirwa aondolewa Ligi Kuu Mwamuzi Ahmada Simba akimuonesha kadi nyekundu mshambuliaji wa Yanga Obrey Chirwa kwenye mechi ya Yanga dhidi ya Ruvu Shooting. Kamati ya Bodi ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi za Tanzania (Kamati ya Saa 72), imemwondoa… Read More
  • Lissu, Masha wanunua kesi ya kupinga uchaguzi TLS   Baadhi ya wagombea wa nafasi ya  urais kupitia kwa chama cha wanasheria wa Tanganyika TLS wanatarajia kuwasilisha maombi ya kujumuishwa kama wadaiwa katika kesi ya kupinga kufanyika kwa uchaguzi wao… Read More
  • Shilole afunguka kuhusu ujauzito   Msanii filamu na muziki wa bongo fleva, Shilole amefunguka na kuweka wazi kuwa yeye hana ujauzito wowote bali ameridhika na maisha jambo ambalo limefanya aongezeke mwili na kunenepa licha ya watu kuwa na hisia ku… Read More
  • Brand New Audio: Mapenzini - Barnaba   Mkali wa  mashahiri ya kubwmbeleza nchi Tanzania Barnaba Classic, ametuletea wimbo wake mpya kabisa unaitwa Mapenzini. … Read More
  • Donald Tusk azua mgawanyiko Poland   Mgawanyiko mpya umetokea ndani ya Umoja wa Ulaya kuhusu kuchaguliwa tena kwa Donald Tusk kuwa Rais wa wa Baraza la Mawaziri. Kukataliwa kwa Tusk na Poland nchi alikotoka hbakujaungwa mkono na nchi wanachama wa Um… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE