December 14, 2015


Kufuatia Mgogoro wa wakulima na wafugaji ulioweza kusababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi wengine wanne wakiwemo askari Polisi wawili katika kijiji cha Dihinda wilayani Mvomero mkoani Morogoro,Hatimaye Waziri wa Kilimo,Uvuvi na Ufugaji Mwigulu Nchemba ambaye amefika eneo hilo amewataka wananchi waache kujichukulia sheria Mikononi.
Kufuatia tukio hilo waziri Nchemba amechukua hatua ikiwemo kuunda kamati za usuluhishi wa migogoro kwa kila kijiji zitakazohusisha pande zote mbili ili kubaini wavamizi wa maeneo na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika na tukio hilo.

 

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE