Wakizungumza katika mashamba hayo, baadhi ya wakulima wameiomba
serikali kuharakisha kutatua migogoro ya ardhi ikiwemo ya wakazi wa
Muheza inayosababishwa na baadhi ya watumishi wake hatua ambayo
imechangia sehemu kubwa ya wanacnhi kuichukia serikali yao kwa sababu ya
watu wachache.
Wakifafanua jinsi walivyopata mashamba hayo baadhi ya wakulima
wakiwemo wazee wamesema wameanza kulima tangu mwaka 1983 chini ya
operesheni nguvu kazi ikiwa ni utekelezaji wa agizo la rais wa kwanza
hayati Baba wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere la kuwataka
wapande mazao ya kudumu ili waweze kujitosheleza kwa chakula.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment