
Diwani wa Ubungo Boniface Jacob kutoka CHADEMA ameibuka kidedea na
ushindi wa kura 38 baada ya kushinda umeya na kumshinda mpinzania wake
Benjamini Sitta wa chama cha Mapinduzi CCM aliyepata kura 20 Kinondoni
jijini Dar es Salaam.Diwani wa Tandale (CUF) Jumanne Amir Mbunju amechaguliwa kuwa Naibu Meya.
Meya
mpya wa Manispaa ya KinondoniBoniface Jacob akiwa mbele ya bara hilo
jipya la Manispaa hiyo mapema leo mara baada ya kushinda kwa nafasi ya
Umeya wa Kinondoni kwa kupata kura 38. Kulia kwake ni Naibu Meya,
Jumanne Mbunju (CUF) ambaye pia ni diwani wa Tandale. Kushoto kwa Meya
ni Mkurugezi wa Manispaa hiyo.
Meya wa Manispaa ya Kinondoni Bw.Charles Kuyeko
Kwa upande wa Umeya kwa
Manispaa ya Ilala imechukuliwa na Charlse Kayoko aliyeweza kunyakua
kura 31 huku upande wa CCM Mgombea wake na wajumbe wake wakikimbilia
ukumbi na kuambulia kura sifuri (0) na kwa upande wa Naibu Meya
ikichukuliwa na Muba Omary (CUF) aliyepata (31) huku naibu aliyegombea
naye kutoka CCM akipata kura sifuri (0).
Kwa hali hiyo Ilala na Kinondoni kwa sasa Mameya wake wanatokea UKAWA huku uchaguzi mwingine unasubiriwa kwa hamu kubwa ni ule wa Meya wa jiji la Dar es Salaam unaotarajiwa kufanyika baada ya wiki moja.
Kwa hali hiyo Ilala na Kinondoni kwa sasa Mameya wake wanatokea UKAWA huku uchaguzi mwingine unasubiriwa kwa hamu kubwa ni ule wa Meya wa jiji la Dar es Salaam unaotarajiwa kufanyika baada ya wiki moja.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment