March 15, 2016

Mtawa 
 Mother Teresa alikuwa mtawa wa kanisa Katoliki 


 Papa 
Mother Teresa na Papa John Paul II wakiwa Kolkata, India tarehe 3 Februari 1986


Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis ametangaza kwamba Mother Teresa atafanywa mtakatifu Septemba mwaka huu.
Sherehe ya kumtawaza kuwa mtakatifu itafanyika tarehe 4 Septemba.
Njia ya kumfanya mtakatifu ilifunguliwa Desemba mwaka jana baada ya Vatican kutambua muujiza wa pili uliohusishwa naye. Muujiza huo alipokea mwanamme raia wa Brazil ambaye alipona saratani kwenye ubongo wake.
Mother Teresa alipewa tuzo ya amani ya Nobel kutokana na huduma yake kwa raia maskini kwenye vitongoji vya jiji la Calcutta nchini India.
Alizaliwa 1910 eneo ambalo kwa sasa hujulikana kama Macedonia na wazazi wa asili ya Albania na kupewa jina Agnes Gonxha Bojaxhiu.
Alipewa uraia kamili wa India baada ya kuanzisha kikundi cha watawa cha Missionaries of Charity mwaka 1950.
Alifariki 1997 akiwa na umri wa miaka 87. Alifanywa mbarikiwa mwaka 2003.

Related Posts:

  • Ugaidi:Tanzania yajiweka katika tahadhari Maafisa wa polisi Waziri wa Mambo ya ndani nchini Tanzania amesema nchi hio ipo katika tahadhari ya juu kufuatia taarifa za vyombo vya habari nchini humo kwamba, kuna uwezekano wa shambilio la ugaidi katika miji ya Dar es sal… Read More
  • Magazeti ya leo April 5/2015 haya hapaIkiwa Leo April 5 2015, wakristu ulimwenguni kote, wanasherehekea kufufuka kwa Yesu Kristu tukimaanisha siku kuu ya Pasaka. Hapa tunakupa fursa ya kupitia vichwa vya habari vya magazeti ya leo. Ubalozini.blogspo… Read More
  • Boko Haram waua watu 20 Nigeriaboko haram Watu 20 wameuawa mashariki mwa Nigeria kufuatia mashambulizi mapya yanayoendeshwa na kundi la Boko Haram katika eneo hilo. Eneo la kwaJaffa, katika jimbo la Borno, lilishambuliwa Jumapili jioni na washambulizi hao … Read More
  • 36 wafariki BangladeshiMvua ya dhoruba kali iliyotokea katika mji wa Dhakanchini Bangladeshi imewauwa watu wapatao 36 na kuwajeruhi watu zaidi ya 200.  Mwandishi wa gazeti la local Prothom Alo ametangaza… Read More
  • ACT: Tunajipanga kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Agosti Dar es Salaam.Chama cha ACT- Tanzania, kimesema hakina muda wa kufanya siasa za chuki na malumbamo dhidi ya vyama vingine vya siasa, badala yake kinajipanga vizuri na kuandaa mazingira ya kushiriki katika uchaguzi mkuu ujao… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE