March 16, 2016

                        

Aliyekua kiungo wa Arsenal, Emmanuel Petit ameungana na mashabiki waliochoshwa na utawala wa meneja wa klabu hiyo Arsene Wenger, kwa kumtaka akae pembeni na kuwapisha wengine.

Petit, ambaye aliwahi kutwaa ubingwa wa ligi ya nchini England (Premier League) pamoja na kombe la chama cha soka nchini humo (FA Cup) mara mbili chini ya Wenger, amekubaliana na msukumo ambao umekua ukitolewa na mashabiki kwa kumtaka mzee huyo wa kufaransa kuondoka.

                      

Amesema imekua ni vigumu kuwamini kama Wenger anaweza kubadilisha muelekeo wa mafanikio kwenye klabu hiyo kwa sasa, na kwake anaona ni wakati mzuri kwa meneja huyo aliyedai anamuheshimu kumpisha mtu mwingine ili akalie kiti chake.

Petit, ambaye kwa sasa anafanya shughuli za uchambuzi wa soka katika kituo cha televisheni cha Canal+ cha nchini kwao Ufaransa, amesisiza kuwa, hakuna njia mbadala kwa Wenger kutwaa ubingwa wa England ama ule wa barani Ulaya kwa sasa kutokana na ushindani kuendelea kukua siku hadi siku, na wakati mwingine huamini mbinu zake zimepitwa na kasi ya michuano hiyo.

Amedai kwamba kushindwa kutetea ubingwa wa kombe la FA baada ya kutolewa na Watford mwishoni mwa juma lililopita, ni ishara tosha ambayo inamuaminisha yeye kama mchezaji aliyewahi kucheza chini ya urtawala wa Wenger, hakuna zuri lijalo kwa Arsenal zaidi ya kuendelea kupata aibu ya kumaliza msimu huu bila chochote mkononi.

Mtazomo huo wa Petit, unakuwa tofauti ule wa mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Ian Wright, ambaye aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akisema kwamba, Wenger anapaswa kuachwa na kufanya kazi yake klabuni hapo kutokana na kuwa ufanisi mkubwa.

Wright, alikwenda mbali zaidi kwa kuwataka mashabiki wanaompinga babu huyo, kuacha kabisa kufanya hivyo, kutokana na makubwa aliyoifanyia klabu hiyo hadi kufikia hatua ya kumiliki uwanja mkubwa kama wa Emirates uliopo kaskazini mwa jijini London.

Purukushani za mashabiki kumtaka Wenger aondoke ziliibuka kufuatia matokeo mabaya yanayowaandama kwa sasa, huku wengine wakichukizwa na mazuri yanayoonekana kwa Leicester City, ambayo wanaamini yalipaswa kuwa upande wa The Gunners.

Leicester City, inaendelea kujiwekea mazingira mazuri ya kutwaa ubingwa wa nchini England kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu hiyo, huku ikiwa imeiacha Arsenal kwa tofauti ya point 11, kwenye msimamo wa ligi.

Related Posts:

  • Diamond aburutwa Mahakamani na Hamisa Mobetto Mwanamitindo Hamisa Hassan Mobetto amemfungulia kesi ya madai mzazi mwenzie, Msanii Naseeb Abdul @diamondplatnumzkwa madai ya kushindwa kumuomba radhi pamoja na kutotoa fedha za matunzo ya mtoto wao, Abdul Naseeb Juma.… Read More
  • IGP Sirro ataka mjadala wa Tundu Lissu ufungwe Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Simon Sirro ametaka mjadala kuhusu kupigwa risasi kwa mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, ufungwe mara moja. Agizo hilo amelitoa leo akiwa ziarani jijini Mbeya wakati akizungumza… Read More
  • Familia ya Lissu waitaka Polisi kushughulikia swala la Lissu   Familia ya mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu, aliyejeruhiwa na watu wasiojulikana katika shambulia la kujaribu kumuua, wamelitaka jeshi la polisi kutumia ubalozi wa Tanzania nchini Kenya ili kumpata Dereva wa… Read More
  • Huu ndiyo utajiri wa Mwanamuziki AY Msanii wa Bongo Flava, Ambwene Yessaya au maarufu kama A.Y ni moja kati ya wasanii waliopata mafanikio makubwa sana kwenye soko la mziki nchini Tanzania. A.Y ambaye alianza mziki na bado yupo mpaka leo tangu miaka ya 9… Read More
  • Kisarawe wazindua Opereheni ya Ondoa Zero   Mkuu wa Wilaya Mh:Happyness Seneda akizungumza jambo    Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, imezindua Opereshini maalum ya kuhakikisha wilaya hiyo inakuwa ki elimu. Operesheni ondoa zero Kisarawe imezindu… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE