April 24, 2016

Utaratibu mpya bungeni ni wa timu maalum iliyopewa kazi maalum ya kurekodi matukio ya Bunge yote yanayofaa kufikishiwa Wananchi na hayo matukio ndio wanapewa waandishi wa habari ila hakuna tena utaratibu kama wa zamani kwamba kila mwandishi anaweza kurekodi kwa Camera yake chochote anachoona ni habari.
April 24 2016 Jukwaa Huru la Wazalendo Tanzania ‘JUHWATA’ limetoa tamko la mwenendo wa shughuli za bunge ambapo limeiomba Serikali kama wameamua kuzuia bunge kutoonyeshwa pia waache kuonyesha maswala yao ya Kiserikali kuweka usawa na kutoonyesha bunge na badala yake muda huo wananchi wakafanye kazi za kujiingizia kipato badala ya kuangalia vipindi vya live, mbele ya waandishi wa habari kupitia katibu wa Jukwaa hilo, Mtela Mwampamba wameyazungumza haya……….

>>>‘tunaposema kwamba Bunge lisionyeshwe live kwa sababu wananchi wanatakiwa wawe kazini na serikali pia masuala yao ya kiserikali kama ufunguzi wa daraja, ufunguzi wa Mwenge yasionyeshwe nayo live tusubiri yarekodiwe ili wananchi waendelee kufanya kazi, kama wanaonyesha live labda iwe sikukuu ya kitaifa’:-Mtela Mwampamba
Aidha Jukwaa hilo limezungumzia tabia ya baadhi ya wabunge kususia mijadala, vikao na shughuli nyingine za bunge kwa kuwa wamekuwa wakivunja katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara 63 (2) inayozungumzia uwezo wa bunge na majukumu ya bunge wamesema……
>>>’tabia hii ya kuendelea kususa inatunyima fursa sisi wananchi wa kawaida kuweza kujua mawazo mbadala, tumekuwa tunapata mawazo ya upande mmoja kwa sababu upande wa pili umekuwa na tabia ya kususa’ :-Mtela Mwampamba

Source:Millardayo.com

Related Posts:

  • TFF yamtangaza Boniface Mkwasa kuwa kocha mpya wa Taifa Stars Shirikisho la soka nchini, TFF, Jumanne hii limemtangaza rasmi Boniface Charles Mkwasa kuwa kocha mkuu wa Taifa Stars. Mkwasa atasaidiwa na Hemed Morocco kutoka Zanzibar. Taarifa hiyo imetolewa na Rais wa TF… Read More
  • Mzee Yusuph afichua siri ya mchezo Mfalme wa Taarab nchini na kiongozi wa Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuph, amesema sababu za bendi yake kupendwa ni utunzi mzuri wa nyimbo zao. Mzee Yusuph ambaye June 13 kwenye tuzo za muziki za Kilima… Read More
  • AY: awashauri Diamond na Alikiba Rapper Ambwene Yesayah maarufu kama AY ametoa ushauri kwa Diamond na Alikiba kuweka tofauti zao pembeni na kufanya muziki pamoja. AY ametoa ushauri huo baada ya kuulizwa na shabiki kupitia Kikaangoni cha EATV aliyetaka… Read More
  • Happy Birth day to u Zinedine Zidane   Zinedine Zidane a.k.a Zizou amezaliwa June 23 mwaka 1972 na hadi leo amefikisha miaka 43. Zidane ameoa mwaka 1994 mke wake anaitwa Veronique Zidane. Hadi leo wana watoto wanne ambao ni Enzo Fernandez, Theo Zidane,… Read More
  • Ainea kuja na Juddy wiki hii     Mwanamuziki wa kizazi kipya toka mkoani Dodoma Aine wa sinampango naye, yupo mbioni kuachia ngoma yake mpya ya Juddy aliyomshirikisha Dullayo. Akitia Story na blog hii, Ainea amesema ameamua kuja na Dullayo k… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE