Serikali ya China imetangaza kuchukuwa hatua ya kufunga ubalozi wake ulioko nchini Libya kwa muda.
Wizara ya Mambo ya Nje ya China imetoa maelezo kupitia mtandao wa jamii wa Twitter na kutangaza kufunga ubalozi wake wa Libya kwa muda kufuatia ongezeko la mizozo ya ndani.
Maelezo zaidi yanaarifu kwamba baadhi ya maafisa wa kidiplomasia wa China walioko nchini Libya wataendelea kutoa huduma kwa mahitaji ya dharura hadi ubalozi utakapofunguliwa tena upya.
0 MAONI YAKO:
Post a Comment