June 07, 2016



Ndugu zangu waandishi wa habari,
Katika siku za hivi karibuni, Jeshi la Polisi nchini, limepokea taarifa kutoka kwa baadhi ya vyama vya siasa wakitaka kufanya mikutano na maandamano . hata hivyo, Jeshi la Polisi kupitia vyanzo vyake vya mbalimbali vya habari limebaini kuwa mikutano hiyo ina lengo la kuwahamasisha wananchi kutotii sheria za nchi (Civil disorder).

Aidha vyama vingine vya siasa vimeonyesha dhamira ya kupinga kile ambacho kitasemwa na wapinzani wao.

Vyanzo hivyo vya habari vimebainisha kwamba upo uwezekano mkubwa wa kutokea vurugu baina ya makundi mawili ya kisiasa.

Kwa hali hiyo, Jeshi la Polisi nchini linapiga marufuku maandamano na mikutano ya hadhara kuanzia tarehe 07/06/2016 hadi hapo hali ya usalama itakapotengemaa.

Jeshi la Polisi linawataka wanasiasa kuacha mara moja kuwashinikiza wananchi kutotii sheria za nchi.

Jeshi la Polisi halitasita kumchukulia hatua kali za kisheria mtu yeyote au chama chochote cha siasa kitakachokaidi agizo hili.

Aidha Jeshi la Polisi linawataka wananchi kuwa makini na wanasiasa wenye lengo la kutaka kuvuruga amani ya nchi hii na badala yake linawasihi waendelee kushirikiana katika kujenga umoja wa nchi hii.

Asanteni sana kwa kunisikiliza .

Imetolewa na:-
Nsato M. Mssanzya – CP
Kamishina wa Polisi Operesheni na Mafunzo
Makao Makuu ya Polisi.

Related Posts:

  • Move ya kukumbukwa  Kariobu mpenzi msomaji wa ubalozini.blogspot.com. Leo ikiwa ni siku ya jumapili, tumekuwekea move ya Wrong Turn 3: Left for Dead iliyotoka mwaka 2009. Malizia wikend yako kwa kutazama Move hii yua kukumbukwa &nbs… Read More
  • RIWAYA: Mwanafunzi Mchawi ( A Wizard Student ) - Sehemu ya Tisa Mtunzi: Enea Faidy Ilipoishia Sehemu ya 8 ( Bofya hapa Kama Hukuisoma ) ..Mwalimu John alipelekwa makuburini kwaajili ya mazishi ingawa yeye alijiona yuko hai. Dorice alikuwa njiani baada ya kutoroka shulen,… Read More
  • Brand New Audio: Mash J ft G-Nako- Taarifa Mkali wa Hip Hop toka mkoani Morogoro Mash J Mperampera ameachia Audio ya wimbo wake wa Taarifa aliomshirikisha G-Nako. Wimbo huo uliofanywa na Producer Vennt Skillz wa Kwanza Record za Mkoani Morogoro Video yake ilian… Read More
  • Video: Chindo Man ft Wakazi,Fid Q & Dully Sykes – Torati ya Mtaa Ki ukweli kabisa, ukizungumzia makundi ya mziki wa Hip Hop hapa Tanzania lazima hutaacha kulitaja hili kundi la Hip Hop toka Jijini Arusha linaloitwa Watengwa. Sasa hii leo mtengwa Chindo Man ametuletea wimbo wake unaitw… Read More
  • Tazama show ya Jagwa Musi Band   Ni kundi la muziki asili wa Mchiriku toka nchini Tanzania. Ni miungoni mwa makundi machache sana yanayofanya mziki huo wa Mchiriku. Mziki wa Mchiriku ni mziki uliopata umaarufu sana mwanzoni mwa miaka ya 90 mpaka… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE