July 03, 2016

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amepuuzilia mbali madai ya Washington kuwa iko tayari kufanya mazungumzo na Iran juu ya masuala mbalimbali ya kieneo.
Ayatullah Ali Khamenei aliyasema hayo jana jioni alipowapokea wanafunzi wa vyuo vikuu na wakuu wa jumuya za wanachuo wa vyuo hivyo hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haina haja na ushirikiano wa aina hiyo na Marekani na kusisitiza kuwa, lengo kuu la Washington ni kuidhalilisha Iran na kudunisha nafasi yake katika eneo hili.
Kadhalika Ayatullah Khamenei amekosoa vikali mwendo wa kinyonga wa kutekelezwa makubaliano ya nyuklia ya Vienna na kusema kuwa, nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani na Bunge la Kongresi la nchi hiyo zingali zinalitazama taifa la Iran kwa jicho la uadui. Makubaliano ya nyuklia baina ya Iran na kundi la 5+1 maarufu kwa jina la JCPOA yalianza kutekelezwa mwezi Januari mwaka huu ambapo pande hizo mbili ziliahidi kwamba zitatekeleza kivitendo mambo yaliyoainishwa kwenye makubaliano hayo.
Katika mkutano wa jana jioni na wanachuo hapa mjini Tehran, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu aliwapa fursa wanafunzi hao wa vyuo vikuu kueleza matakwa na matarajio yao sambamba na kutoa maoni kuhusu masuala kadha wa kadha ya kitaifa.
Katika hotuba yake pia Ayatullah Ali Khamenei aligusia masuala ya makubaliano ya nyuklia, uhusiano wa nchi hii na Marekani, uchumi wa kimuqawama na mustakabali wa taifa la Iran.

Related Posts:

  • IRAN YALAANI MAUAJI YA WANACHAMA WA HIZBULLH   Mohammad Javad Zarif Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali mauaji ya wanachama sita wa Harakati ya Mapambano ya Lebanon Hizbullah yaliyofanywa na utawala haramu… Read More
  • WANAFUNZI WAPINGA UNYAKUZI WA ARDHI    Polisi nchinikenya katiika mji mkuu Nairobi leo imewafyetulia gesi ya kutoa machozi wanafunzi wa shule ya msingi waliokuwa wakiandamana kupinga unyakuzi wa ardhi waliyokuwa wanatumia kama kiwanja cha kuchez… Read More
  • VIKOSI VYA YEMEN KIHOUTH MJINI SANA'A    Wanamapinduzi wa Kishia wa Ansarullah wa nchini Yemen wamepigana na vikosi vya serikali huko Sana'a mji mkuu wa nchi hiyo. Watu walioshuhudia wamesema kuwa, sauti za risasi na milipuko kadhaa zimesikika huko… Read More
  • ULAYA WAWAPIGIA MAGOTI WAARABU MAPAMBANO YA UGAIDI Mawaziri wa nje wa Umoja wa Ulaya wanakutana mjini Brussels kukiwa na wito ushirikiano wa karibu zaidi kati ya Ulaya na ulimwengu wa Kiarabu katika kukabiliana na makundi ya itikadi kali. Mkuu wa Sera za Nje wa Umoj… Read More
  • New Vide: K-Cee -Turn By Turn      Moja ya wanamuziki wanaofanya poa sana nchini Nigeria na Africa kwa jumla ni huyu jamaa anaitwa K-cee. hapa nakupa firsa ya kuitazama video yake mpya kabisa        &… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE