July 03, 2016

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amepuuzilia mbali madai ya Washington kuwa iko tayari kufanya mazungumzo na Iran juu ya masuala mbalimbali ya kieneo.
Ayatullah Ali Khamenei aliyasema hayo jana jioni alipowapokea wanafunzi wa vyuo vikuu na wakuu wa jumuya za wanachuo wa vyuo hivyo hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haina haja na ushirikiano wa aina hiyo na Marekani na kusisitiza kuwa, lengo kuu la Washington ni kuidhalilisha Iran na kudunisha nafasi yake katika eneo hili.
Kadhalika Ayatullah Khamenei amekosoa vikali mwendo wa kinyonga wa kutekelezwa makubaliano ya nyuklia ya Vienna na kusema kuwa, nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani na Bunge la Kongresi la nchi hiyo zingali zinalitazama taifa la Iran kwa jicho la uadui. Makubaliano ya nyuklia baina ya Iran na kundi la 5+1 maarufu kwa jina la JCPOA yalianza kutekelezwa mwezi Januari mwaka huu ambapo pande hizo mbili ziliahidi kwamba zitatekeleza kivitendo mambo yaliyoainishwa kwenye makubaliano hayo.
Katika mkutano wa jana jioni na wanachuo hapa mjini Tehran, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu aliwapa fursa wanafunzi hao wa vyuo vikuu kueleza matakwa na matarajio yao sambamba na kutoa maoni kuhusu masuala kadha wa kadha ya kitaifa.
Katika hotuba yake pia Ayatullah Ali Khamenei aligusia masuala ya makubaliano ya nyuklia, uhusiano wa nchi hii na Marekani, uchumi wa kimuqawama na mustakabali wa taifa la Iran.

Related Posts:

  • .SHILOLE AINASA, MWENYEWE ATHIBITISHA KATIKA hali isiyo ya kawaida msanii wa filamu na muziki bongo, Shilole, ametangaza kuwa na ujauzito kitu ambacho anaamini kwa kufanya hivyo atapata baraka kutoka kwa mashabiki wake. Mwandishi wa habari hizi … Read More
  • SELE CHID BEENZ BIFU ZITO    Msanii Afande Sele aligeuka mbogo baada kumjibu msanii mwenzake Chid beenz kuwa hawezi kumteka na hana uwezo huo kwani Afande ameshakua mwanajeshi JWTZ na akaacha jeshi hivyo awezi kutishiwa amani n… Read More
  • TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - TAMASHA LA MICHEZO TAMASHA LA MICHEZO LILILOANDALIWA NA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO KWA KUSHIRIKIANA NA UBALOZI WA SERIKALI YA UINGEREZA NCHINI KUPITIA SHIRIKA LA ‘BRITISH COUNCIL’ TAREHE: 27, MACHI, 2012MUDA: 4 Asb- 7… Read More
  • KWA WALE WA MIKOANI Kwa wanunuzi wa jumla Wasiliana na namba hii +255 767 884007 E-mail: Nyumbanilounge@gmail.com… Read More
  • JOBFIRE A.K.A (SAUTI ZA MATUKIO) ASAKA MDHAMINIPICHANI NI MSANII WA MUZIKI WA KIZAZI KIPYA ANAYEJULIKANA KWA JINA LA JOBFIRE A.K.A SAUTI ZA MATUKIO,, NI MZALIWA WA MOSHI MKOANI KILIMANJARO ILA KAZI ZAKE KIMUZIKI ANAFANYIA KISIWANI ZANZIBAR, CHIMBUKO LAKE NI MKOA WA TANGA,… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE