July 03, 2016

Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amepuuzilia mbali madai ya Washington kuwa iko tayari kufanya mazungumzo na Iran juu ya masuala mbalimbali ya kieneo.
Ayatullah Ali Khamenei aliyasema hayo jana jioni alipowapokea wanafunzi wa vyuo vikuu na wakuu wa jumuya za wanachuo wa vyuo hivyo hapa mjini Tehran na kuongeza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haina haja na ushirikiano wa aina hiyo na Marekani na kusisitiza kuwa, lengo kuu la Washington ni kuidhalilisha Iran na kudunisha nafasi yake katika eneo hili.
Kadhalika Ayatullah Khamenei amekosoa vikali mwendo wa kinyonga wa kutekelezwa makubaliano ya nyuklia ya Vienna na kusema kuwa, nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani na Bunge la Kongresi la nchi hiyo zingali zinalitazama taifa la Iran kwa jicho la uadui. Makubaliano ya nyuklia baina ya Iran na kundi la 5+1 maarufu kwa jina la JCPOA yalianza kutekelezwa mwezi Januari mwaka huu ambapo pande hizo mbili ziliahidi kwamba zitatekeleza kivitendo mambo yaliyoainishwa kwenye makubaliano hayo.
Katika mkutano wa jana jioni na wanachuo hapa mjini Tehran, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu aliwapa fursa wanafunzi hao wa vyuo vikuu kueleza matakwa na matarajio yao sambamba na kutoa maoni kuhusu masuala kadha wa kadha ya kitaifa.
Katika hotuba yake pia Ayatullah Ali Khamenei aligusia masuala ya makubaliano ya nyuklia, uhusiano wa nchi hii na Marekani, uchumi wa kimuqawama na mustakabali wa taifa la Iran.

Related Posts:

  • Luis Figo kuwania urais Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Ureno Luis Figo ametoa taarifa za kushitusha baada ya kutangaza kuwania Uraisi wa FIFA. Nyota huyo wa zamani wa vilabu vya Sporting Lisbon, Barcelona, Real Madrid na Inter Milan m… Read More
  • Msafara wa rais wapigwa mawe   Rais Goodluck Jonathan amelaumiwa kwa kukosa kudhibiti kundi la Boko Haram  Msafara wa magari ya Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan umepigwa kwa mawe na watu wanaioishutumu serikali kwa… Read More
  • Tamko la CUF kulaani jeshi la polisi kutumia kuhujumu Demokrasia nchini TAREHE 26-27 JANUARY YA KILA MWAKA CHAMA CHETU KIMEJIWEKEA UTARATIBU WA KUFANYA MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA MATUKIO YA UDHALILISHAJI, UNYANYASAJI NA MAUAJI YALIYOFANYWA NA JESHI LA POLISI NCHINI MWEZI JANUARY MWAKA… Read More
  • Simba yachapwa nyumbani   Simba SC wakimenyana na Mbeya City katika Uwanja wa Taifa jijini Dar. (Picha na Maktaba Yetu) SIMBA SC imeendelea kupoteza michezo yake hasa ya nyumbani baada ya leo kukubali tena kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Mb… Read More
  • Kuelekea maadhimisho ya miaka 10 ya THT, Adam Mchomvu kufanya hili kwa weusi   Nyumba ya Vipaji Tanzania(THT)kuadhimisha miaka 10 tangu kuanzishwa kwake siku ya Jumamosi wiki hii pande za Escape One,Mikocheni jijini Dar   Wasani wa muziki K Star, Baraka Da Prince wakiongozwa na Lamec… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE