July 31, 2016



Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kanda ya Ziwa kimetangaza kufanya maandamano katika kanda hiyo huku wakidai kuyafungia katika mji wa Chato ambao ni nyumbani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli.

Tamko la Chadema limetolewa na Katibu Mkuu wa chama hicho Kanda ya Ziwa Magharibi, Meshack Micus alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake.

“Sisi kama Chadema kanda ya Ziwa hasa kanda ya Victoria tayari tumeshawaelekeza wanachama wetu wote, viongozi wetu wote na tayari mwitikio ni mzuri. Na hadi leo tayari viongozi wetu wa vitongoji 1973 wameshajiandaa wako tayari kwa ajili ya kufanya maandamano na kufanya mikutano ya hadhara katika maeneo yao,” alisema.

“Tutaandaa maandamano kutokea Kyelwa, tutaelekea Misenyo, Bukoba vijijini na tutakuja moja kwa moja mpaka Chato. Na wa Mwanza tayari nimeshawaagiza kwamba maandamano yetu tunaenda kuyafungia Chato,” aliongeza.

Tamko hilo limekuja ikiwa ni siku moja baada ya Rais John Magufuli kuwaonya Chadema kutomjaribu kwa kufanya maandamano bila kufuata utaratibu kwani hatawavumilia.

Rais Magufuli aliwataka wananchi kutokubali kudanganyika na kufanya maandamano na badala yake wajikite katika kufanya kazi itakayowaletea maendeleo.

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alitangaza kile walichokiita ‘Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (UKUTA)’, akiwaalika wafuasi wake kufanya maandamano nchi nzima kuanzia Septemba Mosi mwaka huu.

Related Posts:

  • UNYAMA HUU NI NOMA KWA KWELI Na Haruni Sanchawa MKE wa rais, mama Salma Kikwete alizungumza kweli kwamba, mtoto wa mwenzio ni wako! Lakini sivyo kwa mtoto Suleiman Riziki (4), mkazi wa Pugu Kinyamwezi, jijini Dar es Salaam ambaye amejikuta katika w… Read More
  • KAMA UNATUMIA WHATSAPP BASI HII INAKUHUSU Whatsapp ni moja kati ya makampuni makubwa sana duniani hivi sasa,inadhaniwa kuwa na watumiaji wengi sana duniani hivi sasa kuizidi hata facebook,jambo lililofanya mmiliki wa facebook kuona umuhimu wa kuinunua kwa… Read More
  • DUH!!!! HII INATISHA SASA, KUKUTA JENEZA NJE KWAKO!!!   Mke anasema hii sio mara ya kwanza kwa wao kukuta jeneza dogo likiwa na paka ndani yake ambapo wakati uliopita alichukua hilo jeneza na kwenda kuchoma kisha baada ya siku mbili akakutana na kitu kilekile ml… Read More
  • ONA HUYU DADA ALIVYOADHIRIKA KUTOKANA NA DHALAU Leo Asubuhi Nikiwa Ubungo bus terminal.... Leo asubuhi nikiwa stand ya mabasi ya ubungo,mdada mmoja wakati anapanda kwenye kagari kake akadondosha simu.Mimi nikamuita ili nimweleze kilichotokea,akanisonya tena msonyo wa… Read More
  • SHILOLE KUFANYA BIASHARA   Hit maker wa Nakomaa na Jiji Shilole ame-amplify taarifa za kuhusu kufungua mgahawa wake ambao ameupa jina la wimbo wake mpya uitwao  Chuna buzi cafe anatarajia kufungua mgahawa wake wa chakula maeneo ya nyu… Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE