July 05, 2016

image


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli kwa mamlaka  aliyonayo kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria ya tafsiri za sheria (Interpretation of Laws Act)  Sura 1, leo tarehe 5 Julai, 2016 ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB Prof. William Lyakurwa.
Kufuatia hatua hiyo, kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 9 (2) cha ya Sheria ya mashirika ya umma (Public Corporations Act) Sura 257, Mhe. Rais amemteua Prof. Palamagamba J. A. M. Kabudi kushika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB kwa kipindi cha miaka mitatu.
Kufuatia mabadiliko hayo, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango  kwa mamlaka aliyonayo kwa mujibu wa kifungu cha 48 cha sheria ya sheria ya tafsiri za sheria (Interpretation of Laws Act)  Sura 1,  ametengua uteuzi wa Wajumbe Bodi ya Benki ya Maendeleo ya TIB. Aidha,  kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 9 (1) cha ya Sheria ya mashirika ya umma (Public Corporations Act, Sura 257) Mhe. Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Isdor Mpango ameteua wajumbe wapya wa Bodi wafuatao kwa kipindi cha miaka mitatu:
  1. Gen (Rtd) Mabula Mashauri
  2. Razack B. Lokina
  3. Rose Aiko
  4. Joseph Bwechweshaija
  5. Said Seif Mzee
  6. Arnold M. Kihaule
  7. Maduka Paul Kessy
  8. Charles Singili
Uteuzi  wa Mwenyekiti na Wajumbe wapya wa Bodi unaanza tarehe leo 5 Julai, 2016.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
05 Julai, 2016.

Related Posts:

  • About Life, Na Peace Ze prezdaa Machaku Media, tunakukutanisha na mtangazaji wa kipindi cha Planet Base cha Planet Fm ya Morogoro. Jamaa anaitwa Peace Ze Prezdaa. Hapa licha ya kufanya kipindi cha kiburudani katika radiko, lakini hapa anajaribu kuzungu… Read More
  • Rihanna awauliza mashabiki wake kufuta Snapchat baada ya ...   Last Week End Snapchat got into some serious polemic with it last controversial compaign including Chris Brown and Rihanna. “Would you rather slap Rihanna” or “Punch Chris Brown ?”. Snapchat last ad seriously p… Read More
  • Simba Yang'oka kiume Misri Baada ya wekundu wa msimbazi Simba kutolewa katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika na timu ya Al Masry huku wakitoka sare ya 0 – 0 nchini Misri, afisa habari wa klabu hiyo, Haji Manara amesema kuwa tim… Read More
  • Yanga SC yatangaza kuanza na Tv kisha Radio   Uongozi wa klabu ya Yanga umetangaza kuanzisha vipindi vya michezo vitakavyo ruka katika luninga ya Azam TV kama ilivyo kwa mahasimu wao Simba SC ambao wao tayari walishaanza pamoja na timu ya Azam FC. Wakio… Read More
  • Yanga Yaangamia Botswana Yanga SC yaangukia katika michuano ya kombe la Shirikisho baada ya kutolewa klabu bingwa Barani Afrika dhidi ya Township Rollers FC huko nchini Botswana. Yanga SC imeyaaga mashindano hayo baada ya kulazimishwa sare ya … Read More

0 MAONI YAKO:

Post a Comment

Popular Posts

WADAU

BLOG ZINGINE